• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

"KAMA MNATAKA MALI MTAIPATA SHAMBANI"

Posted on: November 10th, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo, GAIRO 

1,Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,

    Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,

    Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,

    Wakataka na kauli iwafe maishani.

(e. Jabiri Makame, Mkuu wa Wilaya ga Gairo, akikazgu mti wa Parachichi, Kijiji cha Masenge Kata ya Rubeho,alipotembea wanakikundi cha wakulima wa zao la parachichi|)

2. Akatamka mgonjwa, ninaumwa kwelikweli,

   Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali,

   Roho naona yachinjwa, kifo kimenikabili,

   Semeni niseme nini, kiwafae maishani.

3. Yakawatoka kinywani, maneno yenye akili,

    Baba yetu wa thamani, sisi tunataka mali,

    Urithi tunatamani, mali yetu ya halali,

   Sema iko wapi mali, itufae maishani? (P.T)

4. Baba aliye kufani, akajibu lile swali,

    Ninakufa maskini, baba yenu sina hali,

    Neno moja lishikeni, kama mnataka mali,

    Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

5. Wakazidi kumchimba, baba mwenye homa kali,

    Baba yetu watufumba, hatujui fumbo hili,

    Akili zetu nyembamba, hazijajua methali,

    Kama tunataka mali, tutapataje shambani?

6. Kwanza shirikianeni, nawapa hiyo kauli,

   Fanyeni kazi shambani, mwisho mtapata mali,

   Haya sasa buriani, kifo kimeniwasili,

   Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

7. Alipokwisha kutaja, fumbo hili la akili,

   Mauti nayo yakaja, roho ikaacha mwili,

   Na watoto kwa umoja, wakakumbuka kauli,

   Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

8. Fumbo wakatafakari, watoto wale wawili,

   Wakakata na shauri, baada ya siku mbili,

   Wote wakawa tayari, pori nene kukabili,

   Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

(Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Jabiri Omari Makame, akihamasisha Wananchi wa Kijijchi cha Masenge kata yaRubeho juu ya kilimo cha parachichi)

9.Shambani, mbegu nyingi mbalimbali,

   Tangu zile za mibuni, hadi zitupazo wali,

   Na mvua ikaja chini, wakaona na dalili,

   Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

(Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Jabiri Omari Makame, akihamasisha Wananchi wa Kijijchi cha Masenge kata yaRubeho juu ya kilimo cha parachichi)

10. Shamba wakapalilia, bila kupata ajali,

     Mavuno yakawajia, wakafaidi ugali,

     Wote wakashangilia, wakakumbuka kauli,

     Kama mnataka mali, mtayapata shambani.


11. Wakanunua na ng'ombe, majike kwa mafahali,

     Wakapata na vikombe, mashine na baiskeli,

    Hawakuitaka pombe, sababu pombe si mali,

    Kama mnataka mali, mtayapata shambani.


12. Wakaongeza mazao, na nyumba za matofali,

     Pale penye shamba lao, wakaihubiri mali,

     Wakakiweka kibao, wakaandika kauli.

"KAMA MNATAKA MALI MTAYAPATA SHAMBANI".

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa