• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI KUANZISHA CHUO KIKUU CHA KISWAHILI NCHINI

Posted on: August 6th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo

Kutoka:wizara_sanaatz. Agosti 6.2022


Waziri wa Utamaduni, Sanaa Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amekutana na ujumbe wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na ameunda tume kwa ajili ya kuanzisha Chuo Kikuu cha Kiswahili nchini ikiwa ni mkakati kabambe wa kubidhaisha lugha ya Kiswahili katika mabara yote duniani.

Mhe, Mchengerwa ameunda tume maalum ya uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Kiswahili kufuatia ombi lake alilolitoa kwa shirika la UNESCO wakati wa siku ya maadhimisho ya Kiswahili duniani mwaka huu iliyofanyika kwa mara ya kwanza Julai 7, 2022.

Akizungumza mara baada ya mkutano na ujumbe wa UNESCO ofisi za Tanzania leo Agosti 5, 2022 ofisini kwake jijini Dar es Salaam amesema matajio ya Serikali ni kuona kuwa Kiswahili kinavuka mipaka ya Tanzania.

Aidha, Mhe Mchengerwa ameipa tume hiyo siku tano kukamilisha andiko hilo ili liwasilishwe kwenye ngazi za juu kwa ajili ya maamuzi.

Amesema hadi sasa tayari Serikali imetenga na kutoa ekari mia moja kwa ajili ya kujenga chuo hicho ambacho kinatarajiwa kuwa kitalu cha kuzalisha, kuhifadhi na kuendeleza lugha adhimu ya Kiswahili kwenye mataifa mbalimbali duniani.

Amesema katika kikao hicho pamoja na mambo mengine pia wamejadili namna ambavyo wanaweza kuendeleza na kukuza Kiswahili na kuwa nyenzo ya kufundisha lugha ya Kiswahili kwenye lugha nyingine kubwa zakimataifa.

Amefafanua kuwa uanzishwaji wa chuo kama hiki ni jambo ambalo limeshafanyika kwenye mataifa mengine duniani na kuleta mafanikio makubwa hivyo hakuna sababu ya Tanzania kisiwepo, sehemu ambayo ndiyo chimbuko na kiini cha Kiswahili duniani

Amesema namna bora ya kubidhaisha Kiswahili ni kuwa na chuo maalum ambacho kitajikita kwwnye kuendeleza lugha ya Kiswahili na lugha ndogondogo ambazo zimekuwa zikisaidia katika kutoa misamiati kadhaa ya Kiswahili.

Aidha, amesisitiza kuwa chuo hicho kitasaidia kuhifadhi lugha nyingine ndogondogo ambazo zinakwenda kufa ambapo pia kitasaidia kufanya utafiti wa kina kwenye eneo la Kiswahili.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa