• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

10% YA PATO LA NCHI KUTOKA KWENYE KILIMO KUFIKIA 2030

Posted on: August 3rd, 2023

Na. Cosmas M. Njingo. MOROGORO

Agosti 3.2023

Serikali imeendelea kuweka mpango mkakati kwenye sekta ya kilimo ambacho kitachangia 10% ya Pato la Taifa ifikapo 2030 hivyo kukuza uchumi wa Taifa.

Hayo yamesemwa Agosti 1, 2023, mjini Morogoro na Mhe. Mizengo Pinda Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akifungua maonesho ya wakulima na wafugaji maarufu kama Nanenane Kanda ya Mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani Morogoro.

Mhe. Mizengo Pinda alisema Serikali inalenga kuwezesha Wakulima kulima kilimo chenye tija ambacho kitasaidia kuchangia kiasi kikubwa katika pato la Taifa, na kuongeza kuwa Tanzania ina hekta milioni 44 za ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo ambapo, lakini ni  15% ya ardhi hiyo ndiyo pekee inatumika kwa shughuli za kilimo na Mifugo.

“Mpango ambao tunakuja nao Serikali, tunataka tuone unaleta matunda ndani ya muda mfupi kadri itakavyowezekana lakini lengo kubwa mpaka ifikapo 2030 tuwe tumesukuma kilimo kiweze kuchangia angalau 10%...” amesema Mhe. Mizengo Pinda.

Katika hatua nyingine, Mhe. Pinda amesikitishwa na udumavu wa watoto chini ya miaka 5 ambapo mama anakuwa amekosa lishe bora kwa maandalizi ya mtoto kuwa na afya bora, hata hivyo ameweka bayana kuwa Mkoa wa Morogoro una tatizo la udumavu kwa 30.6% ambapo mwanzo ilikuwa 35% ikiongozwa na Iringa yenye 56.9%, wakati Mkoa huo ni Mkoa wa uzalishaji wa chakula cha kutosha katika maeneo mengi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mizengo Pinda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuongeza bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kufikia bilioni 970 huku akitaka fedha nyingi zielekezwe katika Sekta ya kilimo cha umwagiliaji, uzalishaji wa mbegu bora, mbolea na viwatilifu wakati 2022/2023 bajeti ilikuwa bilioni 751.1 na 2021/2022 ilikuwa bilioni 294.2, hivyo kadri miaka inavyozidi kwenda na kasi inaongezeka Zaidi.

Kwa upande wake, Mhe. Adam Kighoma Malima, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro amesema miundombinu kama barabara katika Mkoa huo ni jambo la lazima kwani Mkoa huo umejipanga kuzalisha mazao ya kibiashara ikiwemo mpunga, wakati mkoa huo unauwezo wa kuzalisha tani milioni 2 za zao hilo, hivyo miundombinu ni suala muhimu kwa uchumi wa Taifa.

Naye, Mhe. Abubakar Kunenge Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Maonesho ya Nanenane kanda ya mashariki amesema kanda hiyo imejipanga kufanya vizuri katika sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji kwani kanda hiyo ni kinara wa viwanda vikiwemo viwanda vya sukari na kuwataka wananchi kushirikiana vema na wataalamu ili kulima kilimo chenye tija zaidi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa