• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

DAKTA DUGANGE: MIRADI YOTE IKAMILIKE KWA WAKATI

Posted on: June 20th, 2021

Naibu Waziri Wa Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI Dakta Festo John Dugange amewagiza Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kuhakikisha wanasimamia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi yote na kwamba miradi hiyo inatakiwa kukamilika kwa muda uliopangwa ili ianze kutoa huduma zilizokusudiwa katika kuwaletea maendeleo Wananchi.

Ametoa agizo hilo Juni 20, 2021 katika kikao cha ndani na Viongozi wa Wilaya, Watendaji wa Halmashauri pamoja na watumishi wa Idara ya Afya wakati wa ziara yake kukagua hali ya utekelezaji wa ujenzi wa majengo saba ya Hospitali ya Wilaya ya Gairo pamoja na ujenzi wa boma kwenye zahanati ya Mogohigwa iliyopo kata ya Chigela.

“Nakuagiza Mkurugenzi ukishirikiana na Mwenyekiti wa Halmashauri, hebu kasimamieni kwa ukaribu miradi yote na mhakikishe inakamilika kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na huduma tulizo kusudia hususani kwa hii miradi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na zahanati mpya ya Mogohigwa, lakini pia hata kwa miradi ya urekebishaji miundo mbinu kwenye zahanati za zamani”, alisema Dakta Dugange

Alifafanua kuwa ni lazima pawepo na usimamizi mzuri wa matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za afya kupitia miradi ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya, uboreshaji wa miundominu kwenye kituo cha afya na zahanati pamoja na ujenzi wa zahanati mpya ili thamani ya pesa ilingane na ubora wa majengo yaliyopo na miundo mbinu mingine.

"Mkurugenzi hili nalo ni muhimu sana kulizingatia, Serikali inaleta fedha nyingi kwa ajili ya sekta ya afya, lengo ni kuhakikisha Wananchi wake wananufaika na ubora wa huduma, hivyo thamani na ubora wa majengo pamoja na miundo mbinu yake lazima ilingane kabisa na thamani ya fedha zilizotumika”, alisisitiza.

Kwa upande mwingine alipongeza kasi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na kuemsa kuwa juhudi za Halmashauri zinaonekana ingawa alibaini kasoro ndogo ndogo zilizo jitekeza ambapo alitoa maelekezo kasoro hizo zirekebishwe haraka kwa kipindi cha mwezi mmoja ili huduma zianze kutolewa hususani jengo la maabara ifikapo Julai 20, 201.

Alidai “Umaliziaji siyo mzuri sana, nadhani kulikuwa na shida katika usimamizi kwa mafundi mliowapa kazi hii. Hapa jicho langu lipo kwa Mkurugenzi kama msimamizi Mkuu, Mgangan Mkuu Wilaya na Mhandisi wa ujenzi mmeonyesha udhaifu, ingawa ninawapongeza kwa kasi nzuri ya ujenzi na majengo ni mazuri lakini umaliziaji wake kidogo bado sijaridhishwa nao”.

Aidha kwa upande mwingine Dakta Dugange amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri Bi Agnes Mkandya pamoja na Mweka Hazina Wilaya kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuhakikisha wanafikia lengo la 100% ifikapo juni 30, 2021 kabla yam waka mpya fedha 2021/2022 kuaza.

“Swala la makusanyo kwa Gairo bado mpo chini sana ni 67% tu ya lengo, naagiza pia lipewe uzito zaidi ili kufikia Juni 30, mfike lengo la 100%. Kupitia makusanyo ya ndani mtakuwa na nguvu ya kujiendesha bila kuwa na utegemezi kutoka Serikali kuu, pia itasaidia kuimarisha miundombinu katika utoaji hudumwa kwa jamii’. Alisisitiza Naibu Waziri.

Hata hivyo Dakta Dugange alisisitiza swala la utawala bora, ushirikiano na ushirikishwaji kwa Viongozi kuanzia ngazi ya Wilaya hadi kushuka chini kwenye vivjiji ili kuongeza kasi ya maendeleo badala ya kila mmoja kuzungumza lugha yake hali ambayo alisema inachafua sifa na hadhi ya Wilaya..

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa