• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

DC MAKAME ATAKA USHIRIKIANO

Posted on: June 23rd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Omary Makame amewataka viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), na watendaji wa Serikali kushirikiana na Ofisi yake katika kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya chama tawala ili kuwaletea maendeleo Wananchi badalaya kuendekeza marumbani na majungu yasiyo na tija kwa Jamii.

Alisema hayo Juni 21 alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama za Mapinduzi Wilaya ya Gairo kwenya ofisi za Chama hicho alipofika kwa lengo la kujitambulisha baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogor Mhe. Martine Shigela kufuatia uteuzi wa Wakuu wa Wilaya uliotangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni.

“Sisi sote tunajenga nyumba moja hivyo hatuna sababu ya kugombania fito, tukumbuke lengo letu ni moja tu la kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi la kuwaletea maendelo Wananchi kwa kuhakikisha tunatimiza matarajio yao”, alisema Mhe. Makame.

Alifafanua kuwa msingi wa maendeleo ya Taifa lolote unajengwa katika dhana ya umoja, msikamano, ushurikiano na mahusiano mazuri baina ya viongozi ambao ni watekelezaji wa Sera mbalimbali pamoja na wananchi wenyewe ambao ni wanifaika wa fursa zamaendelo zinazo letwa na serikali kupitia miradi mbalimbali.

“Wananchi wana matarajio na imani kubwa sana kwa Serikali yao katika kuwaletea maendeleo kiuchumi na huduma bora za jamii, hivyo ni lazima sisi viongozi wa juu tushikamane kwa kuzungumza lugha moja kutumia muda mwingi kutafuta njia bora za kutatua kero zao badala ya kila kiongozi kuzungumza lugha yake tofauti na mwenzake”, alitanabahisha.

DC Makame aliahidi kutoa ushirikino wa kutosha kwa uongozi wa CCM Wilaya, sambamba na kuhakikisha ajenda kuu ya kuwahudumia Wana Gairo kwa kusikiliza na kutatua kero zao ili kuwaletea maendeleo anaitekeleza kwa nguvu zake zote kwa kutumia weledi na taaluma aliyonayo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Willaya Mhe. Shabani Sajilo aliezea kufurahishwa kwake na ujio wa Mkuu huo wa Wilaya ya Gairo Mhe. Makame na kueleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kipi tayari kumpa ushirikiano katika kushughulikia kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Sajilo alifafanua kuwa Wananchi wa Gairo ni wachapa kazi na wanabidii ya kujituma katika kuchapa kazi ili kujikwamua kiuchumi lakini changamoto zao hazitatuliwi kwa wakati na viongozi wa Serikali kutokana na marumbano ya mara kwa mara baina ya viongozi hao hali ambayo alisema inakwamisha juhudi za  wananchi kujikwamua.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa