• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

GAIRO KUINGIZWA KWENYE MPANGO WA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

Posted on: October 29th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo

GAIRO, MOROGORO

Oktoba 30.2022

 

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imesema katika mwaka wa fedha uzajo 2023/2024 Wilaya ya Gairo itaingizwa kwenye mpango wa bajeti wa kutekeleza kilimo cha umwagiliaji ikiwa ni mkakati wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia Nchi.

Naibu Waziri wa Kilimi Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB) akihutubia Wananchi wa Kata ya Rubeho wakati akifunga maadhimisho ya Wiki la Kilimo Wilayani Gairo

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB) wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki la Mkulima liliohitimishwa katika kata ya Rubeho Wilayani Gairo Oktoba 29.2022.

“Wiki ijayo nitamuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Umwagiliaji aje hapa kuangalia hayo mabwawa ili mwaka ujao wa fedha 2023/2024 Wilaya ya Gairo tuingize kwenye mpango wa Bajeti ianze kutekeleza kilimo cha umwagiliaji”. Alieleza Mhe. Mavunde.

Naibu Waziri wa Kilimi Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB) akihutubia Wananchi wa Kata ya Rubeho wakati akifunga maadhimisho ya Wiki la Kilimo Wilayani Gairo

Mavunde alisema serikali inaendelea kuweka juhudi mbalimbali za kukabiliana na athari za mabadiliko ya Tabia Nchi, ikiwepo kuwekeza katika miradi ya umwagiliaji ili kuwawezesha wakulima kutoathiriwa na hali ya ukosefu wa mvua na kutegemea mvua za asili peke hali ambayo alisema inapunguza tija katika uzalishaji.

“Serikali inatambua hali ya mabadiliko ya Tabia Nchi, ndiyo maana wataalam wetu watakuja kufanya upembuzi yakinifu na kutoa mapendekezo yatakayosaidia Wizara kutenga bajeti ya uchimbaji mabwawa mapya na kufukua mabwawa yaliyopo, pamoja na kuweka miundombinu muhimu kwa ajili ya kuwezesha Wakuliam wengi zaidi wa Gairo kushiriki kweye kilimo cha umwagiliaji pasipo kutegemea mvua za misimu”. Alibainisha Naibu Waziri Mavunde.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mavinde (kulia) akikabidhi mbolea ya ruzuku kwa mmoja wa wakulima aliyetimiza vigezo na masharti vya kunufaika na mbolea za ruzuku zenye pumgulo la bei ya sh.60,000 kwa mfuko mmoja wa Kilogram 50, wakati wa hitimisho la wiki la Kilimo Kata ya Rubeho Wilaya ya Gairo.

Mavunde akaongeza kuwa Bajeti ya Wizara ya kilimo imeongezeka kutoka Shilingi Bil.294 mwaka 2021/2022 na kufikia kiasi cha shilingi Bil.954 kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Ongezeko ambalo alisema halijawahi kutokea tangia kupatikana kwa uhuru wa Tanzania Bara.

“Ongezeko hili halijawahi kutokea tangu enzi za kupigania Uhuru wa Tanzania Bara mwaka 1961.  Wizara ya Kilimo haijawahi kupoikea fedha nyingi kama ambavyo imepokea katika mwaka wa fedha 2023. Hii ndiyo dhamira ya Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan”. Aliongeza Mhe. Mavunde.

Baadhi ya viongozi Waandamizi ngazi ya Wilya wakiwa na Mhe. Anthony Mavunde wakati wa maadhimisho ya kilele cha Wiki la Mkulima kata ya Rubeho

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe.Jabiri Omari Makame akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mhe. Anthon Mavunde, kufunga Kilele cha Maadhimisho ya Wiki la Kilimo, alisema kupitia Wiki la Mkulima, zaidi ya Wananchi laki moja walishiriki katika maadhimisho ya wiki hilo na kwamba Wakulima na Wananchi wengi wamepata manufaa kutokana na elimu waliyopata kutoka kwa wadau mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri J. Makakme

 “Zaidi wa Wanachi laki moja wameshirikik katika maonesho haya ya Wiki la Kilimo Gairo, ambapo tulitenga viruo vitatu ikiwepo kituo cha Ukwamani Gairo Mjini, Kituo cha Chakwa;e na Kituo cha Rubeho. Mhe Naibu Waziri kupitia Wiki hili lakilimo” alisema

Akaongeza kwamba “Wananchi na wakulima wamepata manufaa mbalimbali ikiwepo Elimu ya kanuni bora za Kilimo, wamepata Mbegu kutoka kwa mawakala wa mbegu waliopo katika viwanja hivi pamoja na mbolea za ruzuku ambazo Serikali imetoa Nchi nzima”.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa