• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

GAIRO MWENYEJI WA MAPOKEZI YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2022 KIMKOA.

Posted on: August 24th, 2022

Na. Cosmas M. Njingo. Gairo Morogoro

Agosti.24.2022

Wilaya ya Gairo imepata heshima ya kuwa Mwenyeji katika mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 kimkoa, ambapo mwenge huo umepokelewa Agosti 24.2022 ukitokea Mkoani Dodoma na kukimbizwa Kiwilaya kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.

(Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (Kulia)Mhe. Fatuma Mwasa, akiwa na Matibu Tawala wa Mkoa Dkt. Mussa Ali Mussa, wakati wa mapokezi ya mwenge wa Uhuru 2022 Kimkoa, Wilayani Gairo)

Akikabidhi Mwenye wa Uhuru 2022 na Wakimbiza Mwenge 6, kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatuma Mwassa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alisema, ukiwa Mkoani Dodoma Mwenge wa Uhuru 2022, Umekimbizwa umbali wa Km 132, umetembelea, na kukagua Miradi 39 yenye thamani ya Sh 14,156, 0000. Pamoja na kutangaza ujumbe wa Mwenge, sambamba na kuhamasisha Wananchi kujitokeza kuhesebiwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi Agosti 2022.

“Mimi Rosemary Senyamule, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, ninakukabidhi Mwenge wa Uhuru 2022 ukiwa salama, unang’ara na unameremeta Mhe. Fatuma Mwassa, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro. Ninakukabidhi wakimbiza Mwenge 6 wa Uhuru Kitaifa, wakiongozwa na Kijana mahiri Sahiri Nyanzabala. Na ninakuombea kwa Mwenyezi Mungu”. Alisema Mhe. Senyamula.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatuma Mwasa akipokea Mwenge huo wa Uhuru 2022 pamoja na Vijana 6 wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa kutoka kwa Mhe. Senyamula, alisema; Ukiwa Mkoani Morogoro Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukimbizwa umbali wa kilometa takribani 2,048,kuona, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 50, yenye thamani ya Sh.13.5 Bilioni.

(Wahe. Wabunge wa Mkoa wa Morogoro wakishiriki mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 Kimkoa, Wilayani Gairo Agosti 24,2022)

“Ninakiri kupokea Mwenge wa Uhuru ukiwa unang’ara na unameremeta. Aidha nakiri kupokwa Wakimbiza Mwenge 6 Kitaifa wakiongozwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 Kitaifa Makamanda wetu Jasiri, Shupavu na Mahiri Sahiri Geraluma”. Alisemma

Na kuongeza “Ukiwa Mkoani Morogoro Mwenge wa Uhuru Unatajiwa kukimbizwa umbali wa kilometa takribani 2, 048,kuonam kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 50, yenye thamani ya Sh.13.5 Bilioni. Nikuahidi kwamba Morogoro tupo timamu, tutaulinda, tutautunza na tutaukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa Ujasiri na ueledi mkubwa”. Alitamba Mhe. Mwasa.

(Mwenge wa uhuru 2022 baada ya kuwasili Wilaya ya Gairo ukitokea Mkoani Dodoma)

Awali Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Sahili Geraluma Nyanzabala, alizitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatekeleza agizo la Serikali la kutenga 10% za mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya kuwezesha kiuchumi Vikundi vya uzalishaji mali vya Wanawake,Vinaja na Watu wenye Ulemavu.

(Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2022, wakiongozwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Nd. Sahili (wapili kushoto)

“Ndugu zangu Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri kote Nchini, Serikali imeagiza kila Halmashauri ihakikishe inatenga 10% kwa ajili ya kuwezesha vikundi vya kiuchumi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu”. Alisisitiza Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Mabadi yaliyoa andaliwa kwa ajili ya utengenezaji wa Majiko katika mradi wa Vijana Kwawalesha kata ya Ukwamani)

Aidha Mwenge wa Uhuru 2022, ukiwa Wilayani Gairo utakimbizwa katika Tarafa ya Gairo, kwenye vijiji 11 kati ya 50 ambapo utapita kwenye miradi 6, kuona kuzindua na kuweka mawe ya Msingi. Miradi hiyo inatajwa kuwa na thamani ya Sh.Bilioni 1,198,476,916.72.

Mhe. Jabiri Omari Makame alitaja Miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru 2022 ni pamoja na Mradi wa Vijana watengeneza Majiko katika Kitongoji cha Kwawalesha, Kata ya Ukwamani wenye thamani ya Sh 21, 439,680, kati ya hizo Sh. 15,000,000 zilizotokana na 4% sehemu ya Mkopo wa 10% kwa Wanawake, Vijana na Wenye Ulemavu.

(Baadhi ya majiko yanayotengenezwa katika kiwanda kidogo cha Vijana watengeneza majiko)

Utazindua Mradi wa ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa shule ya Sekondari Majembwe, wenye thamani ya Tsh.78, 312,830.72, Utaweka Jiwe la Msingi katika Mradi wa ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharula (EMD) wenye thamani ya Tsh.259, 184,378.00.

(Mradi wa ujenzi wa jengo la Wagonjwa wa Dharula, Hospitali ya Wilaya ya Gairo)

Miradi mingine itakayo wekewa Mawe ya msingi ni Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Ramashop-Msingisi (Barabara ya Manyara) iliyojengwa kwa kiwango cha Lami wenye thamani ya sh. 247,637,790.00 fedha za Tozo ya miamala ya simu, na Mradi wa Kituo cha kuuzia mafuta (MC Petro Station), wenye thamani ya Sh.318, 000,000.

Pia Mwenge wa Uhuru 2022 utaweka Jiwe la Msingi katika Upanuzi wa Mradi wa Maji Makuyu kwenda Kinyolisi na Iyogwe, wenye thamani ya sh. 288, 336, 896.95, kisha utafuatiwa na Mkesha wa Mwenge wa Uhuru kwenye Viwanja vya Gairo ‘A’ shule ya Msingi, ambapo Agosti 25, Mwenge wa Uhuru 2022, utakabidhiwa Wilaya ya Kilosa.

(Mradi wa vyumba 4 vya madarsa shule ya sekondari Majembwe)

(Kuweka jiwe la msingi barabra ya Ramashio-Msingisi Guest (Barabara ya Manyara)

(Upanuzi wa Mradi wa Maji Kinyolisi, Makuyu hadi Iyogwe)

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa