• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

GAIRO YAFULULIZA KUPATA HATI YA KURIDHISHA MIAKA MINNE (4) UKAGUZI WA HOJA ZA CAG

Posted on: June 17th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO DC

Halmashauri ya Wilaya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro imeendelea kufanya vizuri katika kusimamia matumizi ya fedha za umma kwa vipindi vinne mfululizo kwenye utekelezaji wa bajeti kuanzia mwaka wa fedha 2019/2020 hadi 2021/2022 na kupata hati ya kurudhisha kwa mujibu wa Hoja za Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali CAG.

(Mhe. Martine Shugela, Mkuu wa Mkoa wa Morogor akitoa maelekezo kwenye kikao cha baraza maalum la Waheshimiwa Madiwani kujali hoja za Mkagunzi Mkuu na Mdhibiti wa fedha za Umma Juni 18/2022.)

Akitoa salam za Ofisi yake, Mkaguzi na Mdhibi wa Hesabu za Serikali (CAG) Mkoa wa Morogoro, Juni 17, 2022 kwenye Kikao cha Baraza Maalum la Madiwa kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mjini Gairo, alisema Halmashauri zote tisa (9) za Mkoa wa Morogoro ikiwepo Gairo zimekuwa zikifanya vizuri katika kusimamia matumizi ya Fedha za Umma.

"Mhe. Mwenyekiti, nipende kuchukua fursa hii kulipongeza Baraza lako tukufu kwa kazi nzuri inayofanya katika kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha za Umma hasa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Hii imeleta tija kwa Wananchi kwani miradi inaonekana jinsi inavyo wanufaisha, lakini kikubwa zaidi ni kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Gairo ni miongoni mwa Halmashauri tisa (9) za Mkoa wetu wa Morogoro zinazofanya vizuri kwenye eneo hili na zilizopata Hati ya Kuridhisha kwa kipindi cha miaka 4 mfululizo". Alibainisha CAG.

(Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika kikao cha Baraza maalum la waheshimiwa Madiwani kujadili hoja za Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa hesabu za Umma (CAG)


Alisema kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri ya Gairo ilipata jumla ya hoja za ukaguzi 14 kati ya hizo hoja nane (8) sawa na asilimia themanini na nane (88%) zilipata majibu na kufungwa huku hoja 6 sawa na asilimia kumi na mbili (12%) zikiendelea kutafutiwa majibu. Mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya hoja zilikuwa thelathini na nne (34), kati ya hizo ishirini na tisa (29) sawa na aslimia themanini na saba (87%) zimejibiwa na kufungwa ambapo hoja tano (5) sawa na asilimia kumi na tatu (13%) zinaendelea kutafutiwa majibu.

"Mhe. Mwenyekiti mwaka wa fedha 2019/2020 na 2020/2021 jumla ya hoja arobaini  na nane (48) zilihojiwa na ofisi yangu, kati ya hizo hoja thelathini na saba (37) zilijibiwa na kufutwa kabisa, zipo hoja kumi na moja (11) hizi zinaendelea kuhama mwaka hadi mwaka kwani bado hazijapata majibu ya kuziondoa katika kuhojiwa", Alifafanua CAG.

CAG alifafanua zaidi kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo ilihojiwa jumla ya Hoja 25, huku Hoja  kumi na tatu (13) zikipatiwa majibu na kufungwa, wakati hoja kumi na mbili (12) zilizo salia bado zinaendelea kusubiri majibu ili ziweze kuondolewa.

"Mhe. Mwenyekiti, katika bajeti tunayo endelea kuitekeleza ya mwaka wa fedha 2021/2022 ziliibuka jumla ya Hoja ishirini na tano (25), lakini hadi sasa tayari hoja kumi na tatu 13 tumesha ziondoa baada ya kupatikana majibu yake, zimesalia Hoja kumi na mbili tu za ukaguzi ambazo tunaamini Menejimenti ya Halmashauri inaendelea kutafuta majibu yake ili nazo ikiwezekana tuzifunge kabisa". Alisisitiza.

Pichani (kushoto) Mhe. Rachel Myangasi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo (kulia) Mhe. Clement Msulwa, makama mwenyekiyi wa Halmashauri

Kwa upande mwingine CAG aliwataka Waheshimiwa Madiwani hao pamoja na Wataalam wa Halmashauri kuongeza nguvu katika kukusanya mapato kwa kipindi kilichosalia kukamilisha mwaka wa fedha 2021/2022 kuelekea mwaka mpya wa fedha 2022/2023 ili kufikia malengo ya makusanyo iliyojiwekea sambamba na kuendelea kusimamia kikamilifu matumizi yake.

"Niwaombe Waheshimiwa Madiwani na Wataalam wote kwa ujumla kuongeze nguvu na juhudi katika makusanyo ya mapato ya Halmashauri ili lile lengo mlijiwekwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 lifikiwe kuelekea mwaka mpya wa fedha 2022/2023. Muitumie vyema neema ya Mgodi wa Madini ya Dhahabu kule Kitaita". Aliongeza.

Mkutano huo wa Baraza Maalum la Waheshimiwa Madiwani kujadili Hoja za Mkaguzi Mkuu wa Mdhibiti wa Hesabu za Serikali ulihudhuriwa na Mhe. Martine Shigela Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Mariam Ntuguja. Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo Ndugu Shabani Sajilo, Katibu wa CCM Wilaya Bi. Highnes Munisi, Mhe. Jabiri Omari Makame Mkuu wa Wilaya ya Gairo,Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Viongozi wa Dini na Wenyeviti wa Vyama pendwa. 



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa