• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

HOSPITALI YA WILAYA GAIRO YAPOKEA SHEHENA YA VIFAA TIBA, DAWA

Posted on: April 26th, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo

GAIRO, Aprili 26


Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imepokea shehena ya mahitaji mbalimbali ya Vifaa Tiba na Dawa kutoka #BOHARI KUU YA BIDHAA ZA AFYA (MSD) kwa ajili ya Huduma za Afya katika Hospitali ya Wilaya.

Shehena hiyo ya Vifaa Tiba vilivyopokelewa Hospitalini hapo ni pamoja na Vitanda 100, Magodoro 120, Shuka 700 na Dawa za kutibu magonjwa mbalimbali.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Njile Mahela ameishukuru na kuipongeza Serikali ya awamu ya Sita inayaongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Sekta ya Afya Wilayani humo hususani kwa kutenga fedha nyingi za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na kupeleka vifaa tiba na dawa
"Ninaipongeza Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mama yetu Mhe.Dkt Samia, Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwekeza fedha nyingi za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Gairo, pamoja na hii shehena ya Vifaa tiba na Dawa ambayo tumeipokea". Alisema Mganga Mkuu huyo.
Mahela akabainisha kuwa shehena hiyo ya Vifaa Tiba na Dawa, itasaidia kuongeza wigo na kuboresha utoaji wa huduma za Afya Hospitalini hapo kwa kuwa tayari baadhi ya huduma zilishaanza kutolewa.

Akaongeza kuwa pamoja na Serikali kupeleka vifaa Tiba na Dawa Hospitalini hapo, Halmashauri pia ilipokea Wataalam mbalimbali wa afya na Tiba ikiwepo madaktari Bingwa kupitia ajira ya mwaka 2022, na kwamba kwa mwaka huu Serikali inatarajia kuajiri watumishi wengine wa Divisheni ya Afya ambao watapangiwa katika Hospitali ya Wilaya kwa lengo la kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora za Afya na kwa wakati sahihi.
"Kwa sasa Halmashauri yetu tutatembea kifua mbele kwani tunauhakika wakuhudumia wagonjwa wengi kwa wakati mmoja, Dawa zipo za kutosha, Vifaa Tiba tumepata lakini pia tunao wataalam wa uhakika na watakao kidhi mahitaji ndani ya Wilaya yetu na wateja kutoka nje ya Wilaya". Alitamba.
Kwa upande mwingine, Dkt Mahela amewataka wakazi wa Gairo na Wilaya jirani kufika hospitali ya Wilaya kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali za afya, ili kupunguza msongamano katika kituo cha afya ambacho kwa miaka mingi kimekuwa kikitoa huduma kama hospitali ya Wilaya.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa