• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

HUDUMA MPYA YA DAWA KINGA YAANZA KUTOLEWA GAIRO

Posted on: July 13th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO DC

Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kupitia Idara ya Afya imeanza kutoa huduma mpya ya Dawa Kinga ili kusaidia kupunguza ongezeko la maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa makundi mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa kudhibiti UKIMWI upande wa Afya Dakta Lightness Mtaita wa kituo cha Afya Gairo wakati wa kikao cha Kamati ya kudumu ya Kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri kilichofanyika Julai 13.2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

(Wajumbe wa Kamati ya Kudhibiti Ukimwi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo)

“Mheshimiwa Mwenyekit na Wajumbe wa Kamati hii, ninapenda kuwajulisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imeanza kutoa huduma ya Dawa Kinga kwa ajili ya kupunguza maambukizi ya Virus vya UKIMWI, hususani kwa makundi ambayo yanatajwa kuwa kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi”, Alisema Bi. Mtaita.

Alitaja makundi yaliyopo kwenye hatari ya kupata maambukiz ni pamoja na Wanawake wanaofanya biashara ya ngono maarufu kwa dada poa, mapenzi ya jinsi moja hasa wanaume kwa wanaume (Ushoga), Wenza wenye majibu tofauti baada ya kupimwa V.V.U, pamoja na watumiaji wa Dawa za Kulevya kwa kujinga.

“Dawa hizi zitatolewa kwa makundi lengwa ambayo nimeyataja hapo juu, maana tayari yanatambulika kwa kuwa washirika wa makundi hayo wengine nimepata bahati ya kukutana na kuzungumza nao ana kwa ana pamoja na kuwahudumia”. Alifafanua.

(Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika kikao cha Kamati ya Kudhibiti UKIMWI)

Alisema kuwa tabia ya mapenzi ya jinsi moja (ushoga) biashara ya ngono kwa wanawake (dada poa) na matumizi ya Dawa za Kulevya inaanzia ngazi ya familia na kwamba jamii inawatambua watu wa aina hiyo lakini bado haijukui hatua ya kukemea tabia hizo.

“Mheshimiwa Mwenyekiti wengine tunaishi nao kwenye jamii zetu, na tabia hizi zina anzia kwenye ngazi ya familia, hivyo ni wajibu wetu sote kuhakikisha tunashirikiana kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika jamii zetu hasa hasa kwa makundi haya ambayo ndiyo yapo kwenye hatari kubwa ya maambukizi ya IKIMWI”. Alieza.

Kwa upande mwingine Bi. Mtaita aliwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Kudhibiti UKIMWI kuwa zoezi la upimaji wa Virusi vya UKIMWI kwa hiari linaendelea kupitia utaratibu mpya wa Jipime Mwenye (Selftest) ambapo mteja atapewa maelekezo namna ya kutumia kifaa cha kupimia maambukizi hayo kwa njia ya majimaji katika kinywa.

(Mhe. Clement Msulwa (Diwani) Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti UKIMWI)

“Huduma ya kipimo cha Selftest itatolewa kwa wale wasiotaka kwenda kupimwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa kuogopa kujulikana hali zao za maambukizi ya V.V.U, hii inawagusa sana washirika wa ngono (sex partners) ambapo akibainika mmoja kuwa ameathirika atapewa maelekezo ili akawapime washirika wake kwa kutumia kipimo hiki”. Alifafanua Dakta Mtaita.

(Mratibu wa UKIMWI (w) Ndugu Mohamed Amri)

Matangazo ya Kawaida

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari za Gairo December 16, 2022
  • SOMA TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI May 25, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUZOA TAKA, KUFANYA USAFI NA KUKUSANYA USHURU WA USAFI June 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHONGOLO ATIMIZA AHADI YAKE

    February 16, 2023
  • DCC YAPITISHA BAJETI YA SH.1.7 BILIONI

    February 15, 2023
  • WAKANDARASI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UFANISI

    February 14, 2023
  • RAIS SAMIA AWATAKA VIJANA KUWA NA ARI YA KULITUMIKIA TAIFA

    February 11, 2023
  • Tazama zote

Video

MWANASHERIA MSOMI AAMUA KUUZA JUISI MITAANI
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA SITA 2022 GAIRO SEKONDARI
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa