• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

HUDUMA ZA WAVIU GAIRO ZABORESHWA, VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA VYAFIKA 6 KUTOKA KITUO KIMOJA.

Posted on: December 2nd, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

Gairo, MOROGORO.

Disemba 2.2022.

Katika kupambana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na UKIMWI, huduma zimeendelea kuboreshwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kuwawezesha Watu wanaoishi na Virusi hivyo (WAVIU) kupata huduma bora zinazokidhi mahitaji yao.

Hayo yamebainishwa kwenye risala iliyosomwa mbele ya Mgeni Rasmi Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, Mkuu wa Wilaya ya Gairo, na mmoja wa WAVIU katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani, ambayo kiwilaya yaliazimishwa katika kijiji cha Leshata kata ya Leshata Disemba 1.2022.

“Katika kupambana na V.V.U na UKIMWI, utoaji wa huduma kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI imeboreshwa hasa kwenye vituoa vya ushauri nasaha, Upimaji wa V.V.U, upimaji wa CD4 na utoaji wa Dawa za kufifisha makali ya V.V.U; pamoja na kuongeza vituo vya kutolea huduma hizo”. Ilisema sehemu ya Risala hiyo.

Kwa mujibu wa Risala hiyo kwa Mgeni Rasmi, hapo awali WAVIU walikuwa wakikabiliwa na upungudu wa vituo vya kutolea huduma, ambapo kulikuwa na kituo kimoja tu, ambacho ni Kituo cha Afya Gairo. Hali ambayao iliwalazimu kusafiri umbali mrefu kwenda kutafuta huduma hizo na kuwasababishia usumbufu mkubwa.

“Uboreshaji wa huduma kwa WAVIU ni pamoja na kuongeza vituo vya kutolea ushauri nasaha, vipimo na ugawaji wa dawa za ARV (CTC), kutoka kituo kimoja hadi vituo sita. Hii imetupunguzia kero ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma hizo, mfano wengine tulikuwa tunatoka kata za mbali kwenda kituo cha Afya Gairo”. Ilisema Risala hiyo.

Vituo vitano vilivyo ongezeka kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha huduma kwa WAVIU ni pamoja na Zahanati za Rubeho, Msingisi, Kibedya, Chakwale na Zahanati ya Chogoali, na kwamba uwepo wa vituo hivyo umerahisisha upatikana wa huduma kwa WAVIU waishio katika kata hizo na kata za jirani.

Kuhusu hali ya unyanyapaa, risala hiyo ilibainisha kwamba vitendo vya unyanyapaa kwa WAVIU bado vinaendelea licha ya elimu kutolewa kwa umma ya kupinga vitendo vinavyoashirikia unyanyapaaji; lakini vitendo hivyo vinajitokeza kwa baadhi ya jamii kuwanyanyapaa Watu wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi, na upande mwingine WAVIU wamekuwa na tabia ya kujinyanyapaa wao wenyewe.

Risala hiyo imeeleza kuwa kutokana na vitendo vya unyanyapaa kuongezeka, waathirkika wengi wameshindwa kujitangaza kuhusu afya zao; na kwamba hali hiyo inachangia WAVIU wengi kuishi na msomgo wa mawazo na kusababisha kupoteza maisha mapema.

Aisha katika Risala yao WAVIU hao wameishauri Jamii na Wadau wote kwa ujumla kujitokeza kupima Afya zao kwa hiari, sambamba na kuimba Serikali kusaidia upatikana wa usafiri ili kuuwezesha uongozi wa KONGA kutekeleza majukumu yao ya kutoa elimu kwa umma juu ya kudhibiti maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI.

 Siku ya UKIMWI Duniani huadhimishwa Disemba Mosi kila mwaka, ambapo kwa Mwaka huu kilele cha Maadhimisho hayo Kitaifa kimefanyika Mkoani Lindi, na Mgeni Rasmi akiwa ni Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Matangazo ya Kawaida

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari za Gairo December 16, 2022
  • SOMA TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI May 25, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUZOA TAKA, KUFANYA USAFI NA KUKUSANYA USHURU WA USAFI June 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YATAKA UFANISI KATIKA UFUATILIAJI WA MAREJESHO YA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    December 07, 2022
  • WAGANGA WAKUU, WAFAMASIA WA HALMASHAURI WAHIMIZWA KUZINGATIA TARATIBU ZA UTOAJI DAWA

    December 06, 2022
  • SHERIA NDOGO YA KUDHIBITI SUMUKUVU KUWABANA WAKULIMA, WAUZAJI, WASAMBAZAJI, WASINDIKAJI WA MAZAO.

    December 05, 2022
  • WANAOISHI NA ULEMAVU, WAASWA KUTOJITENGA NA JAMII INAYOWAZUNGUKA

    December 03, 2022
  • Tazama zote

Video

VIBE LA MAKARANI WA SENSA GAIRO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA SITA 2022 GAIRO SEKONDARI
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa