• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

IDARA YA ELIMU MSINGI GAIRO YAPATA GARI JIPYA LA TSH 92.346 MILIONI

Posted on: June 22nd, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro imepokea gari lenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 92,346,913.16 kwa ajili ya uboreshaji na kuimarisha ukaguzi, ufuatiliaji, usimamizi wa shughuli mbalimbali za Idara ya Elimu Msingi pamoja na utekelezaji wa miradi ya Elimu.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Afisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bwana Cosmas Njingo, Afisa Elimu Msingi Bwana Zakayo Mlenduka alisema Gairo ni Miongoni mwa Halmashauri 184 Tanzania Bara zilizo pewa magari hayo kutoka Serikali Kuu kwa kushirkiana na Mradi wa EP4R.

“Magari haya yalitolewa Mwezi Mei 2021 na Mhe. Kasimu Majaliwa Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ikishirikiana na Mradi wa EP4R ambao ni wadau wakubwa kwa Elimu nchini wamesaidia jumla ya Halmashauri 184 tanzania Bara”, alisema Bwana Mlenduka.

Afisa Elimu Msingi Bwana Mlenduka libainisha kuwa Gari hilo limekuja wakati muafaka kwani kwa kipindi kirefu sana Idara ya Elimu Msingi ilikuwa ikikabiliwa na changamoto ya usafiri wa uhakika hali ambayo alisema ilikwamisha kutekeleza majukumu ya idara yake na kwamba changamoto hiyo imepata ufumbuzi.

Alisema “Kwa kweli tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hasssan, Rais wa Jamhuri yauungano wa Tanzania kwa kutuongezea nguvu kwani kwa kupata gari hili shughuli na huduma za idara zitaimarika sana pia itakuwa rahisi kwetu kutembelea shule zilizopo pembezoni mwa mji wa Gairo na kutatua kero mbalimbali za walimu kule kule mashuleni badla ya kusubiri walimu waje makao Makuu ya Halmashauri kuleta malalamiko yao:.

Aliongeza kuwa Serikali imetoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu ikiwepo ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo na ofisi za walimu lakini miradi mingi ilikuwa ikitekelezwa chini ya kiwango kutokana na idara hiyo kushindwa kutemnbelea miradi hiyo kwa ajili ya kukagua, kufuatilia na kusimamia utekelezaji wake.

 “Kimsingi kwetu kupata Gari hili ni fursa kubwa sana ya kutuwezesha kufanya ufuatiliaji wa karibu, kusimamia na kukagua shughuli za ujenzi wa miradi yote inayotekelezwa na Idara ya elimu Msingi kwa kuwa miguu ya kutembea na kufika popote kwa muda mfupi tunayo baada ya Serikali kutuongezea nguvu kupitia gari hili”, alitanabaisha.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa