• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII KUSAJILI VIJIWE VYA WAENDESHA BODA BODA

Posted on: July 20th, 2021

Na. Cosmas Njingo-GAIRO DC

Idara ya maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro imejipanga vyema kuanza utaratibu mpya wa kutambua na kusajili vikundi vya vijana waendesha pikipiki maarufu bodaboda kwenye kata zao kupitia Watendaji wa Kata ili kurahishisha zoezi la kutambua vikundi vinavyohitaji kupewa mkopo wa 4% unaotolewa kwa ajili ya vijana.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Mohamd Amri amesema hayo kwenye kikao cha waendesha boda boda Wilayani humo kilicho itishwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabiri Makame na ofanyika katika ukumbi wa Diana Julai 19.2021.

“Mhe. Mkuu wa Wilaya, idara ya maendeleo ya Jamii imejipanga kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata katika zoezi la utambuzi wa vijiwe vyote vya waendesha boda boda Wilaya nzima ili kujua idadi ya vijana katika kila kijiwe kwa ajili ya kupanga utaratibu mzuri wa utoaji wa mikopo kwa vikundi vitakavyo kidhi vigezo”, alisema Ndugu Amri.

Alisema zoezi hilo litafanyika kwa muda wa majuma mawili (siku 14) likienda sambamba na usajili wa idadi ya vijana ambapo kila kijiwe kitasajiliwa na kutambulika rasmi chini ya Halmashauri pia kupitia mfumo huo itakuwa rahisi kwa idara hiyo kuendesha mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali ili kuviwezesha vikundi hivyo kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi.

“Tunaimani siku 14 zinatosha kabisa kufanya utambuzi wa vikundi vyote, hii itatusaidia kujua kijiwe kipi kina idadi ya boda boda wanagapi lakini pia idara ya Maendeleo ya jamii itaweza kuwafikia kwa urahisi hasa kupitia programu ya mafunzo na elimu ya ujasiriamali kwa vijana “, alisisitiza.

Akafafanua zaidi kwamba yamekuwepo malalamiko mengi kuhusu ucheleweshaji wa utaratibu wa kutoa mikopo kwa makundi ya vijana, wanawake na wenye ulemavu ambapo alisema tatizo kubwa linatokana na ufinyu wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwani ndiyo hugawanywa kwenye mikopo ya makundi hayo.

“Kwanza utaratibu wa kuchakata mikopo kwa haya makundi unategemea sana vyanzo vya ndani vya Halmashauri, lakini pia vipo vikundi ambavyo tayari vilishapewa mikopo na vinaendelea kurejesha kulingana na makubaliano yaliyopo kwenye mikataba, vikimaliza marejesho ndio vikundi vingine vitapewa mkopo kwa kuzingatia maombi”, alisema.

Aidha alibainisha kuwa Halmashauri inaendelea kutekeleza malekezo ya Serikali ya kuhakikisha inayafikia makundi yote yanayo stahili kupewa mkopo wa 10% ambapo alisema 4% zinaelekezwa kwa wanawake na vijana huku 2% zikilekezwa kwa wenye ulemavu na kwamba zaidi ya shilingi milioni 30 zimshatolewa kwa vikundi mbalimbali ikiwepo kikundi cha Rubeho Transporters ambacho kilikopeswa pikipiki 10 zenye thamani ya shilingi milioni 23 na laki tano.

Awali baadhi ya waendesha boda boda hao walilalamika kwa Mkuu wa Wilaya kuwepo kwa urasimu katika utaratibu wa upatikanji wa mikopo kwenye ofisi za Halmashauri, huku wakieleza kwamba wametuma maombi yao kwa muda mrefu lakini kila wanapo fuatilia wanajibiwa warudi kesho.

Mmoja wa vijana hao alisema” Mheshimiwa kuna tatizo kubwa pale Halmashauri, idara ya maendeleo ya jamii wanatuzungusha tunapo fuatilia maswala ya mikopo tunaambiwa rudi kesho, njoo kesho, hii hali inakutatisha tamaa sana hadi tumeamua kuachana na hiyo biashara ya mikopo”.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabir Makame alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Agnes Mkandya kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii kuhakikisha vikundi vyote vya waendesha boda boda vinasajiliwa na kutambulika rasmi sambamba na kuviwezesha kujikwamua kiuchumi kwa kuharakisha upatikanaji wa mikopo.

 

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa