• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAIMU DED GAIRO AWATAKA WAKUU WA IDARA NA VITENGO,MAAFISA BAJETI KUANDAA BAJETI KWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VINAVYO TEKELEZEKA KATIKA MPANGO WA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: December 16th, 2021

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Hamlashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Susan Nyanda amewataka Wakuu wa Idara na vitengo na Maafisa bajeti wa kila idara kushirkiana na watendaji wengine katika idara zao kuandaa na kupanga kwa pamoja mpango wa bajeti inayotekelezeka sambamba na kuweka vipaumbele katika bajeti ijayo kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Ametoa wito huo Disema.17.2021 wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi ya siku 2 juu ya Mfumo wa PlanRep iliyoboreshwa kwa ajili kuandaa mpango wa bajeti za idara mbalimbali za Halmashauri kuelekea upangaji wa bajeti mpya kwa mwaka wa fedha 2022/2023, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

“Mtumie fursa hii muhimu kujifunza kisha mkakae pamoja na watumishi wengine katika idara zenu ili muanda bajeti inayotekelezeka kwa kuzingatia mahitaji muhimu na kuweka vipaumbele vitakavyo tumika kwenye maandalizi ya bajeti mpya katika mwaka wa fedha ujao wa 2022/2023”, alielekeza Bi. Nyanda.

Kaimu Mkurugenzi Nyanda akatumia nafasi hiyo kuwaonya washiriki wa mafunzo hayo kuacha tabia ya kutoka toka kwenye chumba cha mafunzo, na badala yake wawe watulivu, waongeze usikivu na umakini pindi wawasilishaji wanapoelekeza hatua muhimu za kufuata katika mchakato wa kuandaa bajeti kupitia mfumo huo mpya wa PlanRep iliyoboreshwa.

“Nina wataka mtulie na muwe makini sana kwa kipindi chote cha mafunzo, punguzeni kutoka toka nje ili msipitwe na mwendelezo wa mada, nisingependa kusikia malalamiko kutoka kwa wazeshaji kuwa kuna hali ya utovu wa nidhamu au watu kutotulia kwenye chumba cha mafunzo”, alionya Kaimu Mkurugenzi Nyanda.

Naye mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo Bwana. Mussa Mshana aliwambia washiriki hao kuwa swala la kupanga bajeti na kusimamia utekelezaji wake siyo jambo la Afisa Mipango bali ni swala la idara husika moja kwa moja, hivyo ni vyema kila idara ikapanga bajeti kwa kuweka vipaumbele muhimimu vinavyotekelezeka ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza wakatai wa kutekeleza bajeti hiyo.

“Naomba nisisitize kuwa bajeti siyo ya Afisa Mipango wa Wilaya. Hapa ijulikane kuwa mmiliki mkuu na mtekelezaji namba moja wa bajeti ni Mkuu wa Idara husika na watumishi waliopo katika idara hiyo, hivyo niwajibu wenu kukaa pamoja kwenye idara zenu na kuweka vipaumbele vinavyokubalika na vinayotekelezeka”, alifafanua Bwn. Mshana.

Mafunzo hayo ya siku 2 yameanza Disemaba 17 na yatakamilika Disemba 18.2021, yanaedeshwa na Maafisa wawezesha kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikioa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa lengo la kuawjegea uwezo wakuu wa idara na vitengo pamoja na watumishi wengine kuwa na stadi muhimu za namna ya kuandaa bajeti kwa kuzingatia vipaumbele vya idara vinavyotekelezeka kuelekea kwenye maandalizi ya Mpango wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Miongoni mwa wawezeshaji wanaoendesha mafunzo hayo ni pamoja na Mchumi kutika OR-Tamisemi Bwana Adlrahiman Khatibu, Afisa TEHAMA Bi. Esther Mussa na Bwana Mussa Mshana, ambapo imeelezwa kuwa baada ya mafunzo hayo washiriki hao watakuwa na ujuzi na mbinu za kutosha kupanga bajeti yenye tija na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za miradi ya maendeleo.




Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa