• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, KILIMO NA MIFUGO YAHIMIZA UHARAKISHWAJI WA UJENZI WA BARABARA YA GAIRO-NONGWE

Posted on: February 17th, 2025

Gairo – Februari 15, 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Kilimo na Mifugo imeahidi kuihimiza Serikali kuharakisha ujenzi wa Barabara ya Gairo–Nongwe ili kuboresha mawasiliano ya barabara na kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji wa mazao ya kilimo katika Kata za Nongwe, Chagongwe na Masenge.

Amesema hayo Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deo Mwanyika (MB), kwa niaba ya wajumbe wa kamati hiyo, wakati wa ziara ya kujifunza fursa zilizopo katika tarafa ya Nongwe, Wilayani Gairo, wakati akihutubia Wakulima wa zao la Parachichi na Viazi Mviringo kijiji cha Mkobwe kata ya Chagongwe, Februari 15.2025.

Mhe. Mwanyika amesema kuwa barabara hiyo ni kiungo muhimu kwa wakazi wa maeneo hayo ambao wanategemea kilimo kama chanzo kikuu cha kipato, na kuongeza kuwa hali duni ya miundombinu ya barabara inakwamisha juhudi za wakulima kufikisha mazao yao sokoni kwa wakati, hali inayosababisha hasara na kupunguza tija katika sekta ya kilimo.

“Tunaihimiza serikali kupitia mamlaka husika kuhakikisha kuwa ujenzi wa barabara hii unapewa kipaumbele cha haraka. Miundombinu bora ya barabara ni kichocheo kikuu cha maendeleo ya viwanda vidogo na kati, hasa vinavyotegemea mazao ya kilimo kama malighafi,” alisema Mhe. Mwanyika.

Ziara hiyo ya Kamati inalenga kutathmini fursa na changamoto zilizopo katika sekta za viwanda, kilimo na mifugo ili kutoa mapendekezo ya kisera na kibajeti yatakayosaidia kuharakisha maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya vijijini.

Wakazi wa tarafa ya Nongwe wameipongeza Kamati hiyo kwa kujionea hali halisi ya miundombinu ya barabara na kutoa wito kwa serikali kutekeleza kwa haraka ahadi hiyo ili kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa jamii.



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA GAIRO LARIDHIA MPANGO NA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 18, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, KILIMO NA MIFUGO YAHIMIZA UHARAKISHWAJI WA UJENZI WA BARABARA YA GAIRO-NONGWE

    February 17, 2025
  • KAMATI YA BUNGE YAHIMIZA WAKULIMA VIJIJI VYA MASENGE, MKOBWE KUPADA MITI

    February 15, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa