• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KASIMAMIENI KWA UKARIBU MIRADI YA ELIMU: DKT. MSONDE

Posted on: August 15th, 2022

Kutoka Tabora

Na. Cosmas M. Njingo. GAIRO DC

Maafisa Elimu Mkoa na Maafisa Elimu Sekondari wa Halmashauri zote Nchini, wametakiwa kuhakikisha wanasimamia na kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya uboreshaji wa miundombinu ya elimu sambamba na kukamilika kwa wakati miradi hiyo kwa lengo la kuepuka hoja za ukaguzi.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu (Elimu) Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Charles Msonde wakati akifungua kikao kazi cha kuwajengea Uwezo Maafisa hao kuhusu Usalama wa Mazingira na Jamii katika kutekeleza miradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari (Tanzania Secondary Education Quality Improvement Project - SEQUIP) kilichofanyika Agosti 15, 2022 Mkoani Tabora.

“Wajibu wenu kama viongozi ni kuhakikisha mnaenda kusimamia kikamilifu utekelezaji wa ujezi wa Miradi ya kuboresha miundombinu ya Elimu, hii itasaidia kupunguza hoja mbalimbali za ukaguzi zinazohusu utekelezaji wa miradi hiyo katika ngazi ya Serikali za Mitaa, husani kwa shule za Sekondari chini ya Mradi wa SEGUIP” Alisma Naibu Katibu Mkuu huyo.

Dkt. Msonde akafafanua kwamba Serikali inaendelea kujenga na boresha miundombinu ya elimu kwa fedha za mradi wa SEQUIP lengo kubwa ni kuboresha elimu ya sekondari, kuongeza fursa ya upatikanaji wa elimu kwa wananfuzni wanaohitimu Elimu ya Msingi na kupata ufaulu unawawezesha kujiunga na kidato cha kwanza, pamoja na  kupunguza vikwazo vinavyosababisha wanafunzi kuacha shule.

“Serikali inaendelea kuwezesha mradi wa SEQUIP ili kuhakikisha miundombinu yote ya shule za sekondari inaboreshwa, lengo la Serikali yetu ni kufungua fursa kwa watoto wetu wapate elimu ya sekondari katika mazingira rafiki, sambamba na kuwaondolea vikwazo vina kuwasaidia wanafunzi kumaliza elimu bora ya sekondari na kupunguza changamoto za upatikanaji wa elimu nchini”. Alisema

Kwa upande mwingine Dkt. Msonde amewataka Maafisa hao kuto kujiingiza katika migogoro ya ardhi inayoweza kusababisha matatizo ikiwepo kushindwa kuendelea na utekelezaji wa ujenzi wa miradi hiyo, na kwamba ni muhimu kujikita kwenye kusimamia ujenzi ili iendane na thamani ya fedha iliyotolewa, pia kusimamia utekelezaji wa ujenzi uzingatie kwa kuzingatia muda uliowekwa ili ikamilike kwa wakati na kutoa fursa kwa Wanafunzi kuanza masaomo haraka.

“Ninyi ni wabobezi katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya elimu, tushirikiane sote kusimamia hii miradi iwe yenye tija katika Taifa letu. Lakini kikubwa zaidi miradi ikamilike ndani ya muda uliowekwa ili watoto wetu wapate fursa ya kunufaika na elimu bora” alifafanua Dkt. Msonde

Akitoa ufafanuzi kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu (Elimu) Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Charles Msonde,  Mkurugenzi Msaidizi Idara Usimamizi wa Elimu Ofisi ya Rais – TAMISEMI Bi. Hadija Mcheka alisema, kikao hicho kimewakutanisha Maafisa elimu hao kwa lengo la kuwajengea uwezo wakasimamia miradi yao kwa weledi mkubwa ambapo mbada mbalimbali zilifundshwa.

“Ndg Naibu Katibu Mkuu Dkt. Msonde kikao hiki ni cha siku mbili, ambapo tunatarajia Maafisa Elimu hawa watapitishwa kwenye mada mbalimbli ambazo zitawasaidia kuwa na uwelewa wa pamoja katika kupanga, kusimamia na kutekeleza maelekezo ya Serikali hususani kwenye usimamizi wa Miradi ya maendeleo”, Alisema Bi. Mcheka.

Aidha alisema Maafisa hao watapata ujuzi wa kitaalam utakaowawezesha kupata mbinu kufahamu taratibu za usimamizi wa miradi na kupata nafasi ya kutoa maoni katika kufanikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi.

Akizungumza kwa niaba ya washirike wenzake Afisa Elimu Mkoa wa Tabora Bw. Juma Kaponda aliipongeza Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu, ambapo waliahidi kwenda kuisimamia na kutekeleza kwa vitendo kwa kuzingatia sheria, miongozo na taratibu zinazowataka ili kuhakikisha sekta elimu ina;eta matokeo chanya kwa Taifa.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa