• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

JABIRI MAKAME AIPONGEZA TBS KWA KUTOA MAFUNZO YA UDHIBITI WA SUMUKUVU KWENYE MAZAO

Posted on: December 2nd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame amelishukuru na kulipongeza Shirika la Viwango Nchini (TBS) kwa kuendesha mafunzo kwa wadau wa kilimo Wilayani humo juu ya udhibiti wa Sumukukuvu kwenye nafaka hasa mahindi na karanga pamoja na bidhaa zake.

Makame ametoa pongezi hizo Disemba 2.2021 katika ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya Udhibiti wa Sumukuvu kwa Wadau mbalimbali wa Kilimo Wilayani Gairo yanayo endeshwa na TBS kwa kushirikiana na Mradi wa TANIPAC uliopo chini ya Wizara ya Kilimo, katika kumbi za Diana, Msufini Pub na Ukumbi wa mikutano Hosipitali ya Wilaya ya Gairo.

“Ninaishukuru TBS kupitia mradi wa TANIPAC chini ya Wizara ya Kilimo kwa kutoa kipaumbele cha kuendesha mafunzo haya muhimu kwa Wananchi wa Gairo kuhusu elimu ya usalama wa chakula hususani katika udhibiti wa Sumukuvu kwenye Mahindi, Karanga pamoja na bidhaa zake”, alishukuru Mhe. Makame.

Makame alisema kuwa Gairo ni miongoni mwa Wilaya 18 nchini zinazotajwa kuwa na tatizo kubwa la Sumukuvu hali ambayo alisema inatishia usalama wa chakula na kuhatarisha afya ya Watumiaji wa nafaka hasa mahindi na karanga.

Alisema “Chakula kisicho salama husababisha madhara ya kiafya na vifo kwa walaji pamoja na athari nyingine za kiuchumi, hivyo ni wajibu wetu sote kuzingatia mikakati ya kukabiliana na changamoto ya Sumukuvu ili vyakula vyetu viendelee kuwa salama kwa muda wote”.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya kusimamia Mradi wa kudhibiti Sumukuvu TBS-TANIPAC Ndugu Jabiri Saleh Abdi alisema changamoto ya sumukuvu ni kubwa kwani inasababisha madhara kwa walaji na kwamba husababisha udumavu kwa watoto wadogo.

“Sumukuvu husababisha madhara makubwa kiafya kwa binadamu na Wanyama ikiwepo magonjwa ya kansa na vifo kwa binadamu, lakini pia hata huleta udumavu kwa watoto wetu kushindwa kuwa na ustawi mzuri katika ukuaji. Nahii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa na Wizara ya Kilimo”, alifafanua Ndugu Abdi.

Uchafuzi wa sumukuvu unatajwa kuenea zaidi katika Mikoa 10 na Wilaya 18 nchini Tanzania ikiwemo Wilaya ya Gairo, ambapo TBS kupitia mradi wa kudhibiti sumukuvu TANIPAC umeanza kutoa mafunzo kwa Wakulima, Wafanya biashara za mazao, wasindikaji wa bidhaa zinazotokana na mahindi na karanga sambamba na wasafirishaji wa mazao kwa lengo la kuhakikisha changamoto hiyo inadhibitiwa kikamilifu.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa