• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2022 KITAIFA, AZITAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUREJESHA 10% ZA MAPATO YA NDANI

Posted on: August 26th, 2022

Na. Cosmas M. Njingo.

Gairo Morogoro

Agosti.23.2022


 

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Sahili Geraluma Nyanzabala, amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatekeleza agizo la Serikali la kutenga 10% za mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya kuwezesha kiuchumi Vikundi vya uzalishaji mali vya Wanawake, Vinaja na Watu wenye Ulemavu.

Ametoa kauli hiyo Agosti 23, 2022 wakati wa mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 Wilaya ya Gairo, na tarehe 24 Agosti 2022 kwenye makabidhiano ya Mwenge kati ya Wilaya ya Gairo na Kilosa yalofanyika kijiji cha Nhembo.

“Ndugu zangu Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri kote Nchini, Serikali imeagiza kila Halmashauri ihakikishe inatenga 10% kwa ajili ya kuwezesha vikundi vya kiuchumi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu”. Alisisitiza Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Makame, akikabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Adamu Iddi mgoyi, alisema Mwenge huo ukiwa Wilayani Kilosa umekimbizwa umbali wa kilometa 179.5 katika kata 9 za Tarafa ya Gairo na miradi 6.

(Kiongozi wa Mbio za Mwnege wa Uhuru Kitaifa Ndg. Sahili Nyanzabala Geraluma akiaga viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Gairo wakati wa makabidhiano ya mwenge huo kati ya Wilaya ya Kilosa na Gairo katika kijiji cha Nhembo Wilaya ya Kilosa)

“Mwenge wa Uhuru 2022, ukiwa Wilayani Gairo, ilikimbizwa katika maeneo mbalimbali umbali wa kilometa 179.5, ambapo uliona, kuzindua na kuweka mawe ya Msingi katika miradi 6,yenye thamani ya Sh.Bilioni 1,198,476,916.72”. Alisema Mhe. Makame.

Agosti 24.2022 Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Jabiri Omari Makame, alipokea Mwenge wa Uhuru Kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatuma Mwasa, ambaye aliupokea Kimkoa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamula.

(Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Adamu Iddi mgoyi, akipokea Mwenge wa Uhuru  2022 kutika kwa Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame)

Aidha ukamilishaji wa miradi hiyo, umechangiwa na fedha za michango kutoka Serikalini Kuu na wadau mbalimbali wa maendeleo. Ambapo Serikali Kuu imetoa kiasi cha Shilingi 856,423,771.05, Mchango wa Halmashauri Shilingi. 16, 377, 239.00, Watu Binafsi Shilingi 318,000,000 na Mchango wa Mwenge Shilingi 1,000,000, na kufanya jumla kuu ya Fedha za michango ywa mwenye kuwa shilingi 1,198,476,916.72.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 Kitaifa alikubali na kupitisha miradi yote iliyotembelewa na mbio na kupongeza Wanagairo kwa mapokezi mazuri na ushirkiano walioutoa wakati wa kukimbiza mwenge Wilayani humo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa