• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAAFISA UGANI KUPEWA VITENDEA KAZI ILI KURAHISISHA UTOAJI WA HUDUMA ZA UGANI KWA WAKULIMA, WAFUGAJI

Posted on: October 27th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo

GAIRO, MOROGORO

Oktoba 27.2022

Serikali inaendelea kuweka mikakati ya kuboreash huduma za ugani kwa kuwawezesha maafisa ugani ngazi za vijiji, kupata vitendea kazi, ikiwepo usafiri ili kuwafikia wakulima na wafugaji kwa haraka zaidi.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Omari Makame

Amesema hayo Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame, katika hotuba yake ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki la Mkulima Wilayani humo Oktoba 27, 2022, kwenye viwanja vyaSoko la Mahindi Kata ya Ukwamani.

Kutoka kushoto: Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Clement Msulwa, Mwenyekiti wa CCM (W) Ndugu Dastan Mwendi, na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame wakisikiliza maelezo kuhusu matumizi ya viwatilifu vya kuulia wadudu kwenye zao la mahindo kutoka kwa Bw. Peter Kihiyo

“Kwa kutambua umuhimu wa Sekta ya Kilimo, Serikali imendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha huduma za ugani, ili wakulima walime kwa tija; Serikali imenunua vitendea kazi vya kutosha zikiwepo pikipiki ambazo watagaiwa Maafisa ugani katika vijiji vyote ili wawe na uwezo wa kuwatembea na kuwafikia Wakulima kwa haraka zaidi”. Alisema Mhe. Makame.

Baadhi ya Wananchi Walioshiriki maonesho ya shughuli za kilimo katika Wiki la Mkulima wakisikiliza maelezo kuhusu matumizi sahihi ya Mbegu za mahindi kutoka kwa Mtaalam wa Kilimo wa ASA

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa, vitendea kazi hivyo, vitarahisisha wakulima wengi zaidi kufikiwa kwa muda mfup,i na kupimiwa udongo, kupewa elimu na ushauri juu ya matumizi bora ya pembejeo, mbole za ruzuku na mbegu bora zinazofaa kutumika kulingana na mazingira waliyopo, ili walime kilimo chenye tija na kuzalisha mazo mengi.

Wnakikundi cha kuzalisha mafuta ya Alizeti cha Chinyankala kutoka kata ya Rubeho, wakionyesha bidaa zao wakati wa Maadhimisho ya Wiki la Mkulima Wilayani Gairo

Akaongeza kuwa wakulima wengi wanazalisha kiasi kidogo cha mazao kutokana na kukosa elimu ya kilimo bora na matumizi ya mbegu sahihi wakati wa kupanda; ambapo wanazalisha kati ya gunia tatu (03) hadi sita (06) kwa heka moja, halia ambayo alisema ni kiwango kidogo sana ingilinganishwa na wakulima wanaofuata kanuni bora za kilimo.

“Nimetembelea baadhi ya vijiji na kuzungumza na Wakulima mbalimbali, kila Mkulima niiyemuuliza anapata mazao kiasi gani anasema anazalisha kati ya gunia tatu hadi sita kwa ekari moja. Hii si sawa kabisa; kwa mkulima anayefuata kanuni bora za kilimo, anauhakika wa kuzalisha gunia ishirini au ishirini na tano katika eneo la ukubwa wa ekari moja”. Aliongeza Mhe. Makame.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame, akitia saini kwenye daftari la wageni alipo tembelea banda la Maonesho ya uzalishaji wa miche ya nyanya inayozalishwa na mjasiliamali Bi. Raha kutoka Msowero Wilaya ya Kilosa, wakati wa madhimisho ya Wiki la Mkulima.

Sambamba la hilo Mhe. Makame akawasisitiza Wakulima kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea za kupandia na kukuzia ili kuongeza rubuta kwenye undogo kwa lengo la kuwezesha mazao kupata rutuba muhimu ya kusaidia ukuaji wake.

 Maadhimisho ya Wiki la Mkulima Wilaya ya Gairo, yalizindiliwa rasmi Oktoba 27.2022, na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Jabiri Omari Makame, ambapo yatafanyika kwa muda a siku tatu hadi Oktoba 30, 2022. Shughuli za maonesho ya bidhaa mbalimbali na teeknolojia za kilimo ziliendelea kufanyika ambapo Wakulima walipata fursa ya kutembelea kwenye mabanda ya wadau wakilimo kujifunza ma kujionea shughuli zinazotekelezwa na Wadau.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame, akikagua moja ya zana zinazotengenezwa na Mzalendo, wakati wa maonesho ya Wiki la Mkulima

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa