• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAAFISA UGANI WATAKIWA KUHAMASISHA WAKULIMA KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAKULMA.

Posted on: October 28th, 2022

Na. Cosmas Mathias Njingo

GAIRO, MOROGORO

Oktoba 28.2022

Maafisa ugani ngazi ya Kata na Vijiji wametakiwa kuhakikisha wanatoa elimu kwa Wakulima na kuwahamasisha kujisajili katika daftari la Wakulima ili kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali ikiwepo pembejeo za ruzuku.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Wiki la Mkulima katika kata ya Ukwamani, ikiambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali za Kilimo.

“Maafisa Ugani ngazi ya Vijiji na Kata chini ya Afisa Kilimo wa Halmashauri, hakikisheni mnawafikia Wakulima na kuwapa Elimu ya umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la wakulima kwani serikali inaleta fedha ili kuwawezesha wakulima kunufaika na fursa mbalimbali ikiwepo unafuu wa upatikanaji wa pembejeo na mbolea za ruzuku”. Alisema Mhe. Makame.

Kwa upande Wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ndg. Dastan Mwendi aliipongeza Serikali kwa juhudi kubwa inazozifanya katika kuwakomboa wakulima hasa kwa kutenga bajeti kubwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kuinua sekta ya Kilimo.

“Ndugu zangu Serikali yetu kupitia Wizara ya Kilimo kwa mwaka huu wa fedha imetenga bajeti kubwa haijawahi kutokea, lengo ni kuhakikisha sekta ya kilimo inainuka na kuwafanya wakulima kupata tija katika uzalishaji. Naipongeza sana Serikali yetu ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassani kwa kipaumbele katika sekta ya Kilimo.

Naye Diwani wa Kata ya Gairo na Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Gairo Mhe. Danistan Mwegoha, alisema maonesho hayo ya Wiki ya Mkulima ni fursa pekee kwa wakulima kujifunza mbinu na kanuni bora za kilimo sambamba na kujionea teknolojia mbambali zinazoweza kumwinua mkulima na kuboresha uzalishaji wa mazao.

“Ninawasihi wakulima kuyatumia vizuri maadhimisho haya ya wiki la Mkulima maana kuna elimu mbalimbali zinatolewa, hii itawasaidia Wananchi kujifunza na kupata uelewa mzuri kuhusu kanuni bora za kilimo cha kisasa sambamba na ufugaji wenye tija”. Alisema Mhe. Mwegoha.

Baadhi ya Taaisi za Kifedha zikiwepo Bank ya CRDB, EQUITY na NMB zimesema zipo tayari kuwakopesha wakulima mikopo yenye riba nafuu ili kuwawezesha kujikwamua kwa kufanya kilimo bora cha kisasa chenye tija.

 Wawakilishi wa Taasisi hizo za kifedha zimedai kuwa zinamuwezesha mkulima kupata Mkopo wa Tekta, fedha taslimu kwa ajili ya kusaidia gharama za kilimo kuanzia usafishaji wa shamba, upatikanaji wa mbegu, mbolea na shughuli zote za shamba hadi kufikia

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa