• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MADEREVA KUACHA KUBUGHUDHI ABIRIA, KUFUATA SHERIA

Posted on: November 23rd, 2022


Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Nov 23.2022.

Viongozi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani wamewataka madereva wa mabasi ya masafa marefu kufuata Sheria ili kuepusha ajali katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Udhibiti Usafiri wa Barabara (LATRA) Bw. Johansen Kahatano na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani SACP Ramadhani Ng’anzi Novemba 23, 2022 walipokutana katika Ofisi za LATRA Mkoa wa Dar es Salaam na kujadili namna bora ya kudhibiti mwendokasi wa mabasi ya masafa marefu kuelekea msimu wa mwisho mwaka.

Aidha, Bw. Kahatano aliwaasa wadau wa sekta ya usafiri ardhini nchini hasa wasafirishaji, madereva, makondakta na mawakala wanaokata tiketi kuzingatia Sheria na kuitii bila shuruti, “sisi hatutakuwa na muhali na mtu yeyote na atakayekiuka Sheria atakumbana na mkono wa Sheria, kwahiyo nawasihi kuwa kila mdau atimize wajibu wake.”

Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi Kikosi ca Usalama Barabarani SACP Ramadhani Ng’anzi alisema kuwa Jeshi hilo limejipanga vizuri kuhakikisha kwamba wale wanaokiuka sheria za usalama barabarani wanachukuliwa hatua bila kuoneana aibu, “Tuna imani kuwa madereva ambao wana leseni na wamepitia katika vyuo vya mafunzo ya udereva watafuata kanuni zinazowaongoza barabarani, sisi kama Jeshi la Polisi hatutosita kuchukua hatua stahiki kwa yeyote atakayebainika anavunja Sheria ya Usalama Barabarani.”

“Tunashukuru wenzetu wa LATRA wameanzisha mfumo wa tiketi mtandao ambao umesaidia sana kudhibiti wale wanaozidisha nauli kiholela na hivyo nawasihi wale wanaokata tiketi wazikate kwa njia ya mtandao. Kwa madereva nawasihi wafuate kanuni na alama zinazowaelekeza barabarani vinginevyo wasije wakatulaumu," alisisitiza SACP Ng'anzi.

LATRA na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabara wanafanya kazi kwa ukaribu kuhakikisha kwamba kunakuwa na udhibiti katika sekta ya usafiri ardhini na hasa katika kuhakikisha kuwa suala la ajali linapungua nchini.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa