• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAFUNZO ELEKEZI KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA

Posted on: June 1st, 2023

Juni 1.2023

Watumishi wa Ajira Mpya Kada mbali mbali walioripoti Halmashsuri ya Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro, wametakiwa kufanya kazi kwa bidii, kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma sambamba na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatatisha ajira zao.

Rai hiyo imetolewa na Afisa Utumishi kutoka Divisheni ya Utawala na Rasimali Watu, Bi. Jane Sanga, wakati wa kikao elekezi kwa watumishi hao, kilichofanyika Mei 29.2023 katika ukumbi mdogo wa Mikutano wa Halmashsuri.

"Kwa hiyo, kila mmoja wenu, anatakiwa kuhakikisha anatekeleza wajibu wake kikamilifu kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu pamoja na kuzingatia taraibu na kanuni za Utumishi wa Umma, pia ni muhimu sana kwa Watumishi wa Umma kujiepusha na vitendo ambavyo vinaweza kusababisha kufukuzwa kazi", alisisitiza Bi. Sanga.

Kwa Upande wake Afisa Tawala Bw. Given William aliwaambia watumishi hao kuzingatia Waraka wa Utumishi Na. 6, wa mwaka 2020 kuhusu Mavazi kwa Watumishi wa Umma unaolekeza aina ya Mavazi yanayotakiwa kuvaliwa na Watumishi wa Umma.

"Waraka wa Utumishi wa Umma Na. 6, wa mwaka 2020 kuhusu Mavazi kwa Watukishi wa Umma unataja bayana aina ya Mavazi yanayotakiwa kuvaliwa na Watumishi wa Umma, lakini pia umeweka makatazo kadha ya aina za nguo ambazo Watumishi wa Umma hawaruhusiwi kuvaa kwenye maeneo ya kazi". Alisema Bw. William.

Afisa Tawala huyo akaongeza kusema "Waraka huu pia umekataza wazi wazi kwa wanawake kuweka rangi kwenye nywele 'yaani brich' na kuchora tattoo. Aidha hairuhusiwi kwa Wanaume kutoga masikio na kuvaa hereni". Alisistiza.

Naye Afisa Tawala II Divisheni ya Utawala na Rasimali Watu Bw. Abuu Liwangira aliwambia Watumishi hao kujenga nidhamu ya kazi na utii, kuwahi kazini kwa muda uliopangwa sambamba na kutoa huduma pasipo upendeleo kwa misingi ya itikadi ya vyama, kabila au dini.

"Tambueni kuwa wajibu wetu ni kutoa huduma kwa watu wote bila upendeleo kwa misingi ya Ukanda au Ukabila, Dini au Itikadi ya chama flani ya cha Siasa Tunatakiwa kuwahudumia Wananchi wote, hii ndio maana ya Utumishi wa Umma". Alisistiza.

Mafunzo hayo yalijumuisha Watumishi Kada ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Mhandisi Ujenzi, Fedha, Manunuzi,Utawala na Usafirishaji

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa