• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MIKAKATI YA SERIKALI KATIKA KUDHIBITI MAGONJWA YA MILIPUKO

Posted on: December 16th, 2022

Na. Asila Twaha,Tanga 

Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya, kutoa elimu kwa jamii na kuweka mikakati thabiti ili kudhibiti uwezekano wa kutokea kwa magonjwa ya mlipuko Nchini.

Hayo yamesemwa na Dkt. James Kengia kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais –TAMISEMI, katika kikao kazi cha Tathmini ya Programu ya utoaji wa Elimu ya Afya na Ushirikishwaji wa Jamii katika Majanga mbalimbali ya magonjwa ya mlipuko kilichofanyika mkoani Tanga Desemba 14, 2022.

“Serikali inaendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kudhibiti magonjwa ya milipuko Nchinim ikiwepo kuhakikisha inatoa elimu ya kutosha kwa Wananchi juu ya kujikinga na Magonjwa yatokanayo na milipuko; sambamba na kuhakikisha tahadhari zote muhimu zinachukuliwa”. Alisema Dakta Kengia.

Dakta Kengia amewataka wataalam wa afya kwa kushirikiana na Wadau wengine ikiwepo Viongozi wa Dini kuendelea kutoa elimu wa jamii ya tahadhali mbalimbali za kujikinga na magonjwa ya milipuko ukiwepo Ukonjwa wa UVIKO-19

"Nitoe rai kwa wataalam wa afya kwa ngazi ya jamii, kuendelea kutoa elimu ya magonjwa ya mlipuko kwa wananchi ili mwananchi aweze kujikinga na magonjwa hayo, katika Ugonjwa wa UVIKO-19 tulishirikiana sana na viongozi wa dini katika kutoa elimu ya tahadhari, tuendelee kushirikiana nao ili tuwe na uwelewa wa pamoja" amesema Dkt. Kengia

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kuimarisha miundombinu kwenye vituo vyote vya kutolea huduma, kununua vifaa tiba pamoja na kuendelea kuajiri wataalam wa afya ili kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Idara ya Afya kutoka Idara ya Kinga Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma; Wizara ya Afya. Bw. John Yuda amesema, Serikali inao wataalamu ambao wanafanya utafiti katika kutafuta kinga na tiba sahihi ya magonjwa ya mlipuko ili kudhibiti maambukizi katika jamii.

“Tunao Wataalam wa Afya wenye uzoefu katika tafiti mbalimbali za kinga na tiba za magonjwa ya milipuko, hawalali wapo kazini muda wote wakiendelea kutafiti kinga na tiba sahihi za magonjwa ya milipuko. Hawa ni watu muhimu sana kwani kupitia tafiti zao watatuletea majibu kamili na kutupatia muongozo namna ya kudhibiti maambukizi katika jamii”. Alisema Dakta Kengia.

Katika maelezo yake, Dakta Kangia; amewataka wananchi kuendelea kuwasikiliza wataalamu wa afya kwa kuchukua tahadhari na kujikinga na magonjwa ya mlipuko ukiwemo ugonjwa tishio wa Ebola ambao uneripotiwa kuenea Nchi jirani ya Uganda.

Naye Mwakilishi kutoka Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais – TAMISEMI Bi. Chipole Mpelembe amesema mafunzo hayo ya siku tatu yatasaidia kuongeza weledi na mbinu bora za kuongeza uwajibikaji katika kudhibiti magonjwa ya mlipuko.

Kikao kazi hicho kimewashirikisha, Wizara ya Afya kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, Waratibu Afya Jamii kutoka mikoa 13 ya Tanzania Bara iliyopo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola, Wadau wa Maendeleo na Watafiti.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa