• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

Posted on: February 19th, 2025

Nongwe, Morogoro – Februari 15, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema kuwa mkoa umejipanga kwa dhati kuhakikisha Wilaya ya Nongwe inakuwa mzalishaji namba moja wa zao la parachichi mkoani humo, kufuatia hali ya hewa ya maeneo ya tarafa hiyo kuonyesha kuafiki ustawi wa zao hilo kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Kilimo na Biashara, wakati wa ziara yao ya kukagua shughuli za kilimo katika Tarafa ya Nongwe, Mhe. Malima alieleza kuwa tayari hatua za utekelezaji wa mpango huo zimeanza kuchukuliwa, ikiwa ni pamoja na kupandwa kwa hekta 227 za parachichi katika maeneo mbalimbali ya tarafa hiyo.

“Mpaka sasa tumeshapanda hekta 227 za parachichi, na tunatarajia kugawa miche 120,000 kwa vikundi vya wakulima ili kuhamasisha kilimo cha kisasa na biashara katika maeneo haya,” alisema Mhe. Malima.

Alibainisha kuwa lengo kuu la mkakati huo ni kuwasaidia wananchi wa Nongwe na maeneo jirani kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo biashara, huku serikali ikitoa msukumo katika kuwezesha upatikanaji wa mbegu bora, pembejeo, pamoja na huduma za ugani kwa wakulima.

Sambamba na jitihada hizo, Mkuu wa Mkoa alisema kuwa Mkoa wa Morogoro pia unaendeleza kampeni ya kuhamasisha uzalishaji wa zao la viazi mviringo (mbatata), ambalo pia linaonyesha mafanikio makubwa katika tarafa hiyo kutokana na rutuba ya udongo na hali ya hewa inayofaa kwa kilimo hicho.

Kwa upande wao, wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge walipongeza juhudi za Mkoa wa Morogoro na kutoa wito kwa serikali kuendelea kuwekeza katika miundombinu, masoko na elimu ya kilimo bora ili kuhakikisha wakulima wanapata faida kubwa kutoka katika kilimo cha parachichi na viazi mbatata..

Ziara hiyo ya Kamati inalenga kuona hali halisi ya utekelezaji wa shughuli za kilimo na viwanda kwa lengo la kuandaa mapendekezo ya kisera yatakayochochea maendeleo ya sekta hizo nchini.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA GAIRO LARIDHIA MPANGO NA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 18, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, KILIMO NA MIFUGO YAHIMIZA UHARAKISHWAJI WA UJENZI WA BARABARA YA GAIRO-NONGWE

    February 17, 2025
  • KAMATI YA BUNGE YAHIMIZA WAKULIMA VIJIJI VYA MASENGE, MKOBWE KUPADA MITI

    February 15, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa