• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKURUGENZI AAGIZA USAFI WA MWISHO WA MWEZI KUFANYIKA KILA WIKI

Posted on: June 6th, 2024


Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Juni 6. 2024Maafisa Watendaji wa Kata Wilaya ya Gairo wametakiwa kutoa elimu na hamasa kwa Umma na kusimamia Wananchi kushiriki zoezi la usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho wa juma badala ya kuwaachia Viongozi wa Serikali kufagia kwenye maeneo yao, ili kuweka mji katika mazingira safi na nadhifu.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Sharifa Nabalang’anya akichangia hija mbalimbali katika kikao cha Kamati ya Lishe Wilaya cha kupitia taarifa za utekelezaji wa Afua za Lishe kwa Robo ya Tatu y kipindi cha Januari-Machi 2023/2024, kilichofanyika Juni 6. 2024 kwenye Ukumbi Mkubwa wa Mikutano wa Halmashauri.

“Gairo yetu ni chafu sana, hapa hapa mjini lakini hata ukitembelea kata za pembezoni nako hali ya usafi haipo vizuri takataka zimezagaa. Tuhakikishe tunasimamia maswala ya usafi, nmeshatoa maelekezo ya maandishi kwa Watendaji wote wa kata kwamba kuanzia tarehe 1 Juni 2024, swala la usafi lifanyika kila jumamosi ya kila wiki’. Alielekeza Bi. Nabalang’anya.

Mkurugenzi huyo alisema kila mwananchi mahala alipo anawajibika kuhakikisha anafanya usafi wa mazingira yake na kuhakikisha anahifadhi taka kwenye vyombo maaluma vya kuhifadhia taka au kusizusanya kwenye maeneo yaliyotengwa aili kurahisisha shughuli za uondoaji wa taka hizo pindi gari inapopita kwa ajili ya kutekeleza zoezi hilo.

Aidha Nabalang’anya alisema kumekuwepo na tabia isiyo faa ya Wananchi kuwaachia Viongozi Waandamizi ndani ya Wilaya, Wakuu wa Taasisi na Watumishi wa Umma kufanya usafi kwenye maeneo ya Wananchi huku wao wakijifungia ndani kusubiri muda wa zoezi la usafi usihe ndio wajitokeze kufungua biashara zao.

“Gairo inashangaza sana, yaani siku za usafi wa mwisho wa mwezi wanaojitokeza kufanya usafi ni Viongozi na Watumishi tena wanawafanyia usafi wananchi wakati huo wenye maeneo maeneo yao wamejifungia ndani kusubiri muda wa kufungua maduka ufike ndiyo watoke, hii ni sawa. Haipendezi usafi wa mazingira uwe unafanywa na Watumishi”. Alisema

Alisema kuwa Timu ambazo zitakuwepo zikiongozwa na Watendaji wa Kata, zihakikishe zinatoa elimu kwa Wananchi na kuwasimamia washiriki kufanya usafi wao wenyewe kwenye maeneo yao kila mwisho wa wiki.

"Haipendezi Viongozi wa Serikali wanaenda kufagia mbele ya duka la Mwananchi. Hilo ni eneo lake anafanya biashara kwa manufaa yake na familia na familia yake, halafu amwachie kiongozi amfanyie usafi. Tunapozungumza Lishe na Afya hatuwezi kuacha kuhimiza maswala ya usafi wa mazingira”. Alisisitiza Mkurugenzi huyo.

Bi. Nabalang’anga akatilia mkazo Zaidi katika kata 3 za mjini ikiwepo Magoweko, Gairo na Ukwamani ambazo ndiyo zimebeba taswira nzima ya Mji wa Gairo, na kwamba maeneo mengi ya kata hizo hususani barabara Kuu ya Morogoro Dodoma yanakabiliwa na takataka nyingi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa