• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKURUGENZI NABALANG'ANYA APONGEZA WALIMU USIMAMIZI WA MIRADI YA BOOST

Posted on: July 2nd, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo, GAIRO

Julai 2.2023

(Ujenzi wa vyumba 3 vya Madarasa na matundu 3 ya Vyoo shule ya Msingi Chinyankala Kata ya Rubeho)

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Bi. Sharifa Nabalang'anya amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali Sekta ya Elimu Awali na Msingi kupitia fedha za BOOST.

Katika ziara hiyo iliyofanyika Juni 30.2023 kwenye kata za Rubeho, Ukwamani, Gairo, Magoweko, Mkalama na Leshata, Mkurugenzi huyo ameridhishwa na hatua mbalimbali za Ujenzi zilizofikiwa na kupongeza juhudi zinazofanyika licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa kwa baadhi ya maeneo ikiwepo changamoto ya upatikanani wa maji.

(Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi Gairo 'A' yenye jumla ya vyumba 14 Elimu Msingi, Vyumba 2 vya Madarasa ya Awali na Matundu 18 ya vyoo)

Akitoa maelekezo ya Jumla, Bi. Nabalang'anya amewataka Walimu Wakuu wa Shule za Awali na Msingi na Wajumbe wa Kamati za Ujenzi kwenye Shule zote zinazotekeleza Ujenzi wa Miundombinu kwa fedha za BOOST, kuimarisha usimamizi na kuongeza ufanisi ili miradi hiyo ikamilike katika ubora wake hasa hatua za umaliziaji wa majengo hayo."Nawapongeza sana wote mmefanya kazi nzuri ingawa natambua kwamba zipo changamoto kadha wakadha katika utekelezaji wa miradi hii. Lakini kikubwa kuliko yote ni Ubora wa Miradi hii. Ni lazima umaliziaje wake uwe katika Ubora wa hali nya juu hasa kwenye upigaji wa plasta na koplo za madirisha" . Alisisitiza Mkurugenzi huyo.

(Ujenzi wa Vyumba 3 vya Madarasa Shule ya Msingi Kitaita kata ya Leshata) 

Bi. Nabalang'anya akatumia fursa hiyo kuelekeza kuwa shughuli za ujenzi ziende sambamba na zoezi la upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira hasa katika maeneo ambayo hayana changamoto kubwa ya maji.Kwa upande mwingine Mkurugenzi huyo amewaagiza Walimu Wakuu wa Shule hizo kihakikisha wanaongeza kasi ya Ujenzi ikiwezeka kazi zifanyike usiku, hivyo maeneo ya utekelezaji wa miradi hiyo yawekewe taa zenye mwanga wa kutosha ili kuwawezesha mafundi kufanya kazi usiku kwa lengo la kufikia muda uliopangwa wa kukabidhi Miradi hiyo.

(Ujenzi wa Nyumba ya Walimu 2/1, pamoja na Vyimba 2 vya Madarasa ya Shule ya Awali Shule ya Msingi Leshata)

 Pamoja naye, Mkurugenzi Nabalang'anya aliambatana na Mkuu wa Divisheni ya Elimu Awali na Msingi Mwl. Emma Kobona, Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji Bi. Msifwahi Haule, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ndg. Cosmas Njingo, pamoja na Mhandisi Ujenzi kutoka Divisheni ya Miundombinu Mijini na Vijijini.

(Ujenzi wa Vyumba 3 vya Madarsa Shule ya Msingi Lukungu Kata ya Ukwamani)


(Ujenzi wa Matundu 3 ya vyoo na Vyumba 3 vya Madarasa Shule ya Msingi Majawanga Kata ya Mkalama)

(Ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa ya Awali, Vyumba14 vya Madarasa ya Shiule ya Msingi na matundu 18 ya Vyoo Yeriko Kata ya Magoweko)

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa