• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VIJANA WA BODABODA WAPATIWA MKOPO WA PIKIPIKI ZA TSH.26 MILIONI, NI SEHEMU YA 10% YA MKOPO WA VIJANA, WANAWAKE, WENYE ULEMAVU

Posted on: July 22nd, 2022

PICHA 1: Diwani  wa Kata ya Kibedya Mhe. Butindi Massatu (mwenye koti la kijani) kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dakta Godbless Luhunga  wakati wa makabidhiano ya pikipiki 10 kwa kikundi cha HUWILA cha bodaboda kutoka kata ya Kibedya


Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO DC

Kikundi cha Vijana wa waendesha pikipiki za kusafiirisha abiria (Boda boda) HUWILA kilichopo kata ya Kibedya Wilaya ya Gairo, kimepokea mkopo unaotokana na 10% ikiwa ni sehemu ya makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri ambazo hurudishwa kwa jamii ili kunufaisha vikundi vya kiuchumi vya Wanawake, Vijana na Wenye Ulemavu.

PICHA 2: Diwani wa Kata ya Magoweko Mhe. Ibrahimu Mmbwana wakati wa makabidhiano ya pipiki 10 za mkopo kwa vijana wa kikundi cha HUWILA zenye thamani ya Ths. 26 milioni.

Kikundi hicho cheye vijana 10 (Me 9 na Ke.1) Kimekabidhiwa jumla ya Pikipiki 10 zenye thamani ya Shilingi 26,000,000 (Milioni ishirini na Sita) ambazo ni 4% zinazoelekezwa kwa Makundi ya Vijana, wakati Wanawake hupewa 4% huku Watu wenye Ulemavu wakipata 2% na kufanya jumla ya mkopo wote kwa makundi hayo kufikia 10%.

Akikabidhi Pikipiki hizo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Rachel Nyangasi, Diwani wa Kata ya Magoweko Mhe. Ibrahimu Mmbwana amewataka Vijana hao kuwa waangalifu na kuzitunza pikipiki ziho ili ziwe na manufaa kwao na kujikwamua kiuchumi.

Diwani wa kata ya Magoweko Mhe. Ibrahimu Mmbwana akiendesha moja ya pikipikii zilizotolewa mkopo kwa kikundi cha Vijana wa HUWILA sehemu ya 10% za mkopo wa vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu

“Ushauri wangu kwenu ni kuhakikisha mnazitunza vizuri hizi pikipiki ili zilete tija kwanu na kwa familia zenu zinazo wategemea. Mkizitunza nao zitawatunza.” Alishauri Mhe. Diwani Mbwana.

Diwani Mbwana aliwambia Bodaboda hao kujiona wao wana bahati kubwa sa kupata mkopo huo kwa wakati huu kwani vipo vikundi vingine vingi ambavyo vimewasilisha maombi ya kupewa mkopo lakini bado havijafanikisha kutimiziwa azima hiyo hivyo ni muhimu kwao kuvilinda vyommbo hivyo sambamba na kulipa mkopo ili kuwezesha vikundi vingine kunufaika na fursa hiyo.

“Msidhani mpo peke yenu wenye sifa za kupata hizi pikipiki, ninyi mna bahati kubwa sana, kwani hata mimi katani kwangu kuna vikundi vingi vimewasilisha maombi Halmashauri ya kupewa Mkopo lakini bado havijafanikiwa, ninaimani mkirejesha kwa wakati pesa za mkopo huu mtawezesha na wengine kupata mkopo hivyo mhakikishe mnakuwa waaminifu katika kurejesha kila mwezi.” Alisistiza.


Naye Diwani wa Kata ya Kibedya Mhe. Butindi Massatu ameishukuru Serikali kwa kuwawezesha vijana hao kupitia mikopo ya 10% inayotolewa na Halmashauri na kuahidi kuwafatilia ili warejeshe mkopo huo kwa wakati uliopangwa.

Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Dkt. Godbless Luhunga amewaasa vijana hao kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuhatarisha usalama wa maisha yao na pikipiki hizo.

Akimkaribisha Nhe. Diwani Ibrahimu kukabidhi pikipiki hizo kwa kikundi cha HUWILA kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri Bi. Rachel Nyangasi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauiri Dakta. Godless Luhunga aliwambiwa vijana hao kuhakikisha wanalinda usalama wa maisha yao na vyombo hivyo kwa kujiepusha na ajali za barabarani.

 “Serikali inawapenda ndiyo maana imewaletea pikipiki hizi, lakini mara zote mkumbuke kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kujihakikishia usalama wa Maisha yenu na vyombo hivi mlivyo pewa ili visilete hasara kwa familia zenu ambazo zinawategemea kwa kiasi kikubwa. Nimuhimu sana kutii sheria bila shuruti, na msiache kuvaa kofia ngumu wakati wote muwapo kazini. Alisema Dakta Luhunga.

Awali Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii (W) Ndg. George Katoto aliwambia Bodaboda hao kukahikishi wanahifadhi pesa kwenye akaunti yao ya kikundi kila wiki na kuwasilisha nakala za malipo hayo kwa Mhasibu wa Kikundi ili kuingiza kwenye daftari la kumbukumbu na kwamba kila mwisho wa mwezi fedha hizo ziwekwe kwenye akaunti ya Halmashauri ikiwa ni marejesho ya kila mwezi ya Mkopo huo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa