• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

ONGEZENI KASI YA UANDIKISHAJI WANANCHI KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA YA iCHF.

Posted on: June 7th, 2024

Na. Cosmas Mathias Njigo. GAIRO

Juni 6.2024 

Wito umetolewa kwa Watendaji wa kata kufanya hamasa na kutoa elimu kwa Wananchi watambue umuhimu wa kujiunga katika Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa iCHF, sambamba na kuongeza kasi ya uandikishaji wa Wanachama wa mfuko huo ili kuwezesha Wananchi wengi kupata huduma za Afya kwa gharama nafuu.

Wito huo umetolea na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Makame, akizungumza na Watendaji wa Kata pamoja na wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya, katika kikao cha Kamati hiyo cha kupitia na kujadilia taarifa za utekelezaji wa afua za Lishe kwa robo ya tatu kipindi cha Januari Machi 2023/2024, kilichofanyika kwenye Ukumbi Mkubwa wa Mikutanao wa Halmashauri Juni 6. 2024.

“Hapa sasa nguvu ya ziada inahitajika, nendeni mkatoe elimu kwa Wananchi kuhusu Bima ya iCHF na kuwahamsisha wajiunge kwa wingi, pia ongezeni kasi kasi ya uandikishaji kwenye vijiji vyote ili Wananchi wajiunge wapate uhakika wa huduma za afya kwa gharama nafuu wakati wowote wanapohitaji kutibiwa”. Alielekeza Mhe. Makame.

Awali Meneja wa iCHF Wilaya ya Gairo Bi. Joanitha Mashasi aliwaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa mojawapo ya changamoto zinazokwamisha zoezi la uandikishaji ngazi za vijiji ni ukosefu Maafisa Waandikishaji wenye uwezo na wanaomiliki simu janja, pamoja naufinyu wa bajeti kununu vitendea kazi hususani Simu janja ambazo zinatumia mfumo wa IMIS kwajili ya uandikishaji na ukusanyaji wa michango ya Wateja.

“Mhe. Mweyekiti Mfumo huu mpya wa iCHF unatakiwa kutekelezwa kwa kutumia simu janja ambazo kimsingi Halmashauri inatakiwa kuzinunua na kuzigawa kwa Maafisa Waandikishaji ngazi za Vijiji, lakini ufinyu wa bajeti umekwamisha kupata simu za kutosha kugawa katika vijiji vyote 53”. Alisema bi Mashasi

Mratibu huyo akaongeza kuwa juhuzi mbalimbali zimefanyika ili kukabiliana na changamoto hiyo kwa kipindi cha mpito, ambapo alitaja kwamba ni kutumia baadhi ya Wahudumu wa Afya waliotayari kutekeleza zoezi hilo kwa kutumia simu zao kufanya uandikishaji katika vituo vya kutolea huduma za afya ngazi za Zahanai, Vituo vya Afya na Hospitali ya Wilaya.

“Changamoto ya ukosefu wa rasilimali watu na vifaa imetufanya kubuni mbinu ya kuwaomba baadhi ya watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya kufanya uandikishaji kwa kutumia simu zao ambazo zimewekewa mfumo wa iCHF, baada ya kuwahamasisha na kuwapa mafunzo ili wasaidie kutekeleza zoezi hilo kwenye vituo vya vya huduma za afya.” Alifafanua Meneje huyo.

Aidha Mkuu wa Wilaya Mhe. Makame amewaagiza Watendaji hao kuanza mchakato wa kuwapata Wananchi ambao wanamiliki Simu janja na ambao wapo tayari kufanya kazi ya uandikishaji wa Wananchi wanaojiunga katika Bima ya iCHF kwani ni sehemu ya kujipatia kipato pia kuongeza idadi ya Wananchama.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa