• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

POLISI GAIRO

Posted on: March 8th, 2023

Jeshi la Polisi Wilaya ya Gairo, limewataka watoto wanaoishi katika mazingira magumu kuishi kwa upendom kujiepusha na dhambi, sambamba na kutoa taarifa dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya kikatili pamoja na kuwafichua wahusika wa matukio hayo.

Hayo yamesemwa Machi 7.2023 na Viongozi Waandamizi Wanawake wa Jeshi hilo wakati wa ziara yao kutembelea Kituo cha Kulelea Watoto wanaotoka katika mazingira magumu na Yatima cha Betheli, ikiwa ni kuadhimisha Wiki ya Wanawake Duniani kuelekea Kilele cha Maadhimisho yako ambayo Kimkoa yatafanyika Wilaya ya Gairo Machi 8.2023.

Kaimu Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Gairo SP WEGESA SANJUKILA amewambia watoto hao kuishi kwa kuzingatia mafundisho ya dini wanayoelekwa na viongozi wa ili kuepuka dhambi.

"Wanangu wazuri mimi ninawaomba muishi kwa kufuata mafundisho ya dini kama ambavyo walimu na viongozi wenu wanavyowaelekeza ili kuimarisha upendo, umoja na mshikamano". Alisema SP SANJUKILA

Mkuu wa Dawati la Jinsia Wilaya wa Jeshi hilo INSP. HOPE TARIMO aliwambia watoto hao kutojiona wanyonge na badala yake wajiamini na kutokubali kudharauliwa na mtu yoyote na kwamba watoe taarifa endapo kuna watu wanataka kuwaonea na kuwatendea vitendo visivyofaa.

"Msikubali mtutu yoyote kuwadharau wala ninyiwenyewe msidharau watu wengine. Mnachotakiwa kufanya kwanza na kujiamini, pia msiache kutoa taarifa dhidi ya matukio ya ukatili na manyanyaso mkiona wezetu wanafanyiwa" Alisema Afande Hope.

kwa upande wake #AFISA POLISI JAMII ASP JOYCE KILIMUGISHA aliataka watoto hao kutoa taarifa sahihi kwa watu sahihi bila woga ili kuliwezesha jeshi hilo kukabiliana nawatu wanaojihusisha na matukio ya ukatili dhidi ya Watoto.

"Mnatakiwa kutoa taarifa sahihi, mahali sahihi na kwa watu sahihi ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wahisika badala ya kutoa taarifa kwa watu wasio husika" alisema ASP Kilimugisha.

Pamoja na mambo mengine Jeshi hilo la polisi likiongozwa na wanawake limetoa msaada wa mahitaji mbalimbali kwa watoto waliopo kituoni hapo ili kuwazesha kujikimu pamoja na kusherehekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani.

Askari hao walikabidhi Mbuzi mmoja kwa ajili ya mboga, mchele kilo 20, mafuta ya kula na viburudisho vingine

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa