• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

PROF. MBARAWA AZITAKA SEKTA BINAFSI KUSHIRIKI UJENZI WA MIUNDOMBINU

Posted on: November 16th, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Nov 16.2022.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amezungumzia umuhimu wa sekta binafsi kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ili kuharakisha maendeleo na kukuza uchumi wa taifa na mtu mmoja mmoja.

Akifungua mkutano wa 15 wa mwaka wa wadau wa sekta ya uchukuzi wenye lengo la kufanya tathmini kuhusu maendeleo ya sekta hiyo nchini, Prof. Mbarawa amesema ushiriki wa sekta binafsi, Serikali na wadau wa maendeleo utaharakisha ujenzi wa reli, barabara, viwanja vya ndege na meli na hivyo kutoa fursa nyingi za ajira na kuhuisha miundombinu ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi wa taifa.

“Serikali tumejipanga kushirikiana na sekta binafsi katika ujenzi wa barabara mpya ya Kibaha-Chalinze-Morogoro kilomita 215 (express way), ambapo mkandarasi atajenga kwa fedha yake na watakaotumia barabara hiyo watalipia,” amesema Prof. Mbarawa.

Amebainisha kuwa Serikali inajipanga kubadilisha Sheria ya TAZARA na TRC ili kuwezesha sekta binafsi kushiriki katika huduma ya usafiri wa reli kwa kununua mabehewa mapya na kuyasimamia ili yawe na manufaa kwa Taifa zima.

Aidha Mhe. Prof. Mbarawa alisema ni muhimu kwa Tanzania kuwa na miundombinu bora kwa haraka ili kumudu kuhudumia kikamilifu soko la ndani la nchi sita ambazo hutegemea huduma ya uchukuzi kutoka Tanzania, ambazo ni Malawi, Zambia, Burundi, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Kingdom Mbangula akizungumzia ujenzi wa barabara mpya ya kulipia, amesema barabara hiyo itakuwa na njia nne, mbili kwenda Morogoro na Mbili kurudi Kibaha na magari hayatapishana ili kuepusha msongamano na ajali.

“TANROADS tumejipanga ipasavyo kuhakikisha mradi huu unajengwa kwa ubora uliokusudiwa na kukamilika kwa wakati,” amefafanua Eng. Mbangula.

Naye Meneja Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Patricia Laverley ameishukuru Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa kuandaa mkutano huo wa tathmini wa kila mwaka ambao unaibua changamoto na kuzipatia ufumbuzi kwa haraka.

Amesisitiza kuwa AfDB imetenga asilimia 60 ya bajeti yake katika uwezeshaji ujenzi wa miundombinu ili kuchochea maendeleo ya uchumi kwa nchi za Afrika.

Katibu Mkuu sekta ya Uchukuzi Bw. Gabriel Migire amesema mkutano huo pamoja na mambo mengine utaibua hoja mbalimbali zinazolenga kuboresha sekta ya uchukuzi nchini hivyo kuvutia wawekezaji wengi kupitisha mizigo yao Tanzania na hivyo kukuza uchumi wa taifa.

Matangazo ya Kawaida

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari za Gairo December 16, 2022
  • SOMA TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI May 25, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUZOA TAKA, KUFANYA USAFI NA KUKUSANYA USHURU WA USAFI June 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YATAKA UFANISI KATIKA UFUATILIAJI WA MAREJESHO YA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    December 07, 2022
  • WAGANGA WAKUU, WAFAMASIA WA HALMASHAURI WAHIMIZWA KUZINGATIA TARATIBU ZA UTOAJI DAWA

    December 06, 2022
  • SHERIA NDOGO YA KUDHIBITI SUMUKUVU KUWABANA WAKULIMA, WAUZAJI, WASAMBAZAJI, WASINDIKAJI WA MAZAO.

    December 05, 2022
  • WANAOISHI NA ULEMAVU, WAASWA KUTOJITENGA NA JAMII INAYOWAZUNGUKA

    December 03, 2022
  • Tazama zote

Video

VIBE LA MAKARANI WA SENSA GAIRO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA SITA 2022 GAIRO SEKONDARI
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa