• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AITAKA MAHAKAMA KUIMARISHA MIFUMO YA UTOAJI HAKI

Posted on: February 1st, 2023
Feb 1.2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kushirikiana na Wizara za kisekta kuzifanyia marekebisho sheria zote zenye mizunguko inayochelewesha kesi na upatikanaji wa haki.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo katika maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali.

Aisha, Rais Samia amesema Sheria mbalimbali zimetoa nafasi ya usuluhishi katika Mabaraza ya Vijiji na Kata hivyo amewataka majaji na Mahakimu kutoa mafunzo kwa kutumia utaratibu wa usuluhishi wa migogoro.

Rais Samia amewaagiza wadau wote katika Sekta ya Sheria kupitia upya taratibu ambazo mashauri hupitia ili kuzifupisha kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa haki kwa haraka.

Vile vile, Rais Samia amesema anatarajia kuona Watanzania wanatambua kwamba kufikishana mahakamani sio jambo la lazima na badala yake usuluhishi iwe ndio njia ya kwanza kutumika.

Rais Samia pia amesema ni lazima mfumo wa utoaji haki unaochukua muda mrefu kutatua migogoro urekebishwe kwa kuwa ni hatari, huongeza gharama na kuathiri mazingira ya uwekezaji na biashara.

Kwa upande mwingine, Rais Samia ameitaka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwachukulia hatua watumishi ambao wanachafua sura na taswira ya muhimili wa Mahakama kwa vitendo viovu vya rushwa, kauli mbaya na hata vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake, watoto na wenye uhitaji maalum.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa