• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AWAHIMIZA WATUNZA KUMBUKUMBU KUZINGATIA USIRI

Posted on: November 27th, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Nov 27.2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo ya kiutendaji ndani na nje ya Serikali ili kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii wanayo ihudumia pamoja na kuepuka malalamiko mbalimbali.

Mhe. Rais Samia ametoa agizo hilo Novemba 27.2022, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Wanataaluma ya Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika Ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Jijini Arusha (AICC).

“Ni wajibu wenu kuhakikisha mnatekelza majukumu yenu kwa weledi na ufanisi wa hali ya juu sana, kwa kuzingatia Sera, Sheria, kanuni na Miongozo mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utoaji wa huduma, na kuondoa malalamiko kutoka kwa Wateja wenu mnao wahudumia”. Aliagiza Mhe. Samia.

Mhe. Rais Samia akaongeza kwa kuwataka Wanataaluma hao wa kutunza kumbukumbu na nyaraka katika ofisi za umma, pamoja na mambo mengine, wanawajibu wa kuhakikisha wanasimamia vyema maadili ya taaluma yao kwa kutunza siri za Serikali, lengo ikiwa ni kuhakikisha nchi inakuwa katika hali tulivu na salama.

“Ninyi ni watu muhimu sana katika Serikali yetu na Taasisi zake zote, hivyo moja ya maadili ya kazi yenu ni utunzaji wa Siri za Serikali. Nendeni mkasimamie vyema maadili ya taaluma yenu, mkihakikisha Siri za Serikali hazivuji vuji hovyo, kuepusha kuleta taharuki kwa Umma, au kuingiza Nchi kwenye machafuko kutokana na ukosefu wa vifua vipana vya kutunza Siri za Serikali”. Alisisitiza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa awamu ya Sita”.

Kwa upande mwingie Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa waajiri Serikalini na Sekta binafsi kuhimiza matumizi ya teknolojia kwenye utunzaji wa kumbukumbu ili kuimarisha mazingira ya kazi kwa kupunguza mrundikano katika vyumba vya masijala.

“Matumizi ya teknolojia katika utunzaji wa kumbukumbu utasaidia kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa haraka pale zinapohitajika k wa ajili ya maamuzi mbalimbali. Na hii itarahisisha sana utoaji wa huduma bora pamoja na kuondoa mrundikano wa majalada vyumba vya Masjala”. Alisisitiza Mhe. Rais.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa