• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AWAHIMIZA WATUNZA KUMBUKUMBU KUZINGATIA USIRI

Posted on: November 27th, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Nov 27.2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo ya kiutendaji ndani na nje ya Serikali ili kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii wanayo ihudumia pamoja na kuepuka malalamiko mbalimbali.

Mhe. Rais Samia ametoa agizo hilo Novemba 27.2022, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Wanataaluma ya Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika Ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Jijini Arusha (AICC).

“Ni wajibu wenu kuhakikisha mnatekelza majukumu yenu kwa weledi na ufanisi wa hali ya juu sana, kwa kuzingatia Sera, Sheria, kanuni na Miongozo mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utoaji wa huduma, na kuondoa malalamiko kutoka kwa Wateja wenu mnao wahudumia”. Aliagiza Mhe. Samia.

Mhe. Rais Samia akaongeza kwa kuwataka Wanataaluma hao wa kutunza kumbukumbu na nyaraka katika ofisi za umma, pamoja na mambo mengine, wanawajibu wa kuhakikisha wanasimamia vyema maadili ya taaluma yao kwa kutunza siri za Serikali, lengo ikiwa ni kuhakikisha nchi inakuwa katika hali tulivu na salama.

“Ninyi ni watu muhimu sana katika Serikali yetu na Taasisi zake zote, hivyo moja ya maadili ya kazi yenu ni utunzaji wa Siri za Serikali. Nendeni mkasimamie vyema maadili ya taaluma yenu, mkihakikisha Siri za Serikali hazivuji vuji hovyo, kuepusha kuleta taharuki kwa Umma, au kuingiza Nchi kwenye machafuko kutokana na ukosefu wa vifua vipana vya kutunza Siri za Serikali”. Alisisitiza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa awamu ya Sita”.

Kwa upande mwingie Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa waajiri Serikalini na Sekta binafsi kuhimiza matumizi ya teknolojia kwenye utunzaji wa kumbukumbu ili kuimarisha mazingira ya kazi kwa kupunguza mrundikano katika vyumba vya masijala.

“Matumizi ya teknolojia katika utunzaji wa kumbukumbu utasaidia kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa haraka pale zinapohitajika k wa ajili ya maamuzi mbalimbali. Na hii itarahisisha sana utoaji wa huduma bora pamoja na kuondoa mrundikano wa majalada vyumba vya Masjala”. Alisisitiza Mhe. Rais.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni

Matangazo ya Kawaida

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari za Gairo December 16, 2022
  • SOMA TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI May 25, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUZOA TAKA, KUFANYA USAFI NA KUKUSANYA USHURU WA USAFI June 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YATAKA UFANISI KATIKA UFUATILIAJI WA MAREJESHO YA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    December 07, 2022
  • WAGANGA WAKUU, WAFAMASIA WA HALMASHAURI WAHIMIZWA KUZINGATIA TARATIBU ZA UTOAJI DAWA

    December 06, 2022
  • SHERIA NDOGO YA KUDHIBITI SUMUKUVU KUWABANA WAKULIMA, WAUZAJI, WASAMBAZAJI, WASINDIKAJI WA MAZAO.

    December 05, 2022
  • WANAOISHI NA ULEMAVU, WAASWA KUTOJITENGA NA JAMII INAYOWAZUNGUKA

    December 03, 2022
  • Tazama zote

Video

VIBE LA MAKARANI WA SENSA GAIRO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA SITA 2022 GAIRO SEKONDARI
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa