• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA MGENI RASMI KONGAMANO LA HABARI, KIKAO KAZI CHA MAAFISA HABARI

Posted on: June 17th, 2024

Na. Cosmas Mathias Njingo, DAR ES SALAAM

Juni 17. 2024

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anatarajwa kuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Kikao cha 19 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Itifaki wa Serikali, ambacho kitatanguliwa na Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari Nchini tarehe 18-19 Juni 2024.

Mbali na Rais Samia, viongozi wengine watakaoshiriki ni pamoja na Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu wa Wizara na Manaibu Katibu Wakuu, Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Habari Maelezo, baadhi ya Wakuu wa Taasisi za Umma, Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini, Wahariri na Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari.

Kikao hicho ambacho kimeratibiwa na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kinalenga kuwajengea uwezo Maafisa Habari, Mawasiliano na Itifaki hao wa Serikali, kuwaongezea waledi kwa kuwapa mbinu mpya jinsi ya kufikisha taarifa kwa uma kuhusu utekelezaji wa shughuli za Serikali ngazi ya Wizara, Taasisi za Umma, Mikoa Majiji na Halmashauri, sambamba na kuongeza ubunifu katika kutekeleza wa majukumu yao ya kila siku.

Kwa mwaka 2024, kikao kazi hicho cha 19 kitafanyika kwa siku 3 kuanzia tarehe 20-24 Juni.2024, huku kikiwa kimebeba Kaulimbiu inayosema "Jenga Mustakabali Endelevu kwenye Sekta ya Habari katika Zama za Kidijiti" ambayo inawakumbusha Wadau wote wa Sekta ya Habari na Mawasiliano kutumia fursa ya Teknolojia katika kuchochea maendeleo na kukuza uchumi kwa kupashana habari zenye tija kwa Umma, sambamba na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii hasa katika kipindi hiki ambacho dunia inaendeshwa Kidijiti.

Wadau wote wa Sekta ya Habari wanatarajiwa kuungana kwa pamoja katika Ukumbi wa Mikutano wa  Mlimani City Jijini Dar es salaam, ili kujadili mafanikio, changamoto na mikakati ya kuimarisha na kuboresha Sekta hiyo kwa maslahi mapana ya Taifa, kwa kuzingatia kuwa Sekta ya Habari na Mawasiliano ni Sekta mtambuka inayotegemewa na Wadau mbalimbali na Taifa kwa ujumla, kuleta mabadiliko chanya kiuchumi, kifikra na kijamii.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa