• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI, SEKTA BINAFSI ZAINGIA UBIA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAJI GAIRO

Posted on: May 27th, 2024

Na. Cosmas Njingo. GAIRO

Mei 27/2024

Imeelezwa kuwa malengo ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeingia makubaliano na Sekta binafsi ya kuhakikisha inaondoa kero ya Maji kwa Wananchi wa Gairo mradi utakaotekelezwa na pande hizo mbili.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame, akifungua warsha ya siku moja ya kutambulisha mpango huo kwa Wadau wa Sekta ya Maji, iliyofanyika Mei 25/2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri, ambapo Mradi huo unaotarajiwa kutekelezwa Wilayani Gairo kwa Ubia wa Serikali na Sekta Binafsi,

Makame alisema kuwa ni kuhakikisha inaboresha na kuimarisha huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama ni ya uhakika na inapatikana karibu na makazi ya Wananchi.

 “Serikali yetu inayoongozwa na Mhe. Dakta Samia Suluhu Hassan inayo nia ya dhati ya kumtua Mama ndoo kichwani kwa kuhaikisha inaboresha na kuimarisha huduma za uhakika za upatikanaji wa maji safi na salamani karibu na makazi ya wananchi”. Alisema Mhe Makame.

Mkuu huyo awa Wilaya akaongeza kuwa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaitaka Serikali kuhakikisha inaondoa kero ya Maji kwa Wananchi ifaikapo 2025, kwa kuhakikisha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama Mijini inafika 95% na 85% upate wa vijijini.

Akitoa Salam za Chama, Mwemyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo Ndg. Danistan Daudi Mwendi, alimpongeza Mhe. Samia Rais wa Jamhuri ya Tanzania kwa kuendelea kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwepo mradi huo wa Maji.

“Nichukue fursa hii kipekee kabisa kutuma salamu zangu za pongezi kwa niaba ya Chama change cha Mapinduzi Wilaya ya Gairo na Wananchi wote wa Gairo, kwa Mhe. Rais Samai kutokana na uchapakazi wake mahiri. Gairo tunaendelea kupokea fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za miradi”. Alisema

Naye Kaimu Katibu wa CCM Wilaya Ngd. Mbarouk Soggo ameipongeza Wizara ya Maji na taasisi zake zote zinashughulika na utekelezaji wa Miradi mbalimbali maji kwa lengo la kuhakikisha Wananchi Wananufaika na huduma bora za upatikanaji wa Maji ya uhakika safi na salama, na kwamba kazi kubwa ya Serikali ni kuhakikisha Wananchi wa mijini na Vijijini wanaondokana kabisa na kero ya ukosefu wa maji safi na salama Wilayani Gairo.

Kwa Upande wake Mweyekiti wa Halmashauri Mhe. Rahel Nyangasi ameupongeza uongozi wa Mamlaka ya maji Mjini (MORUWASA) kwa kuendesha Warsha hiyo muhimukwa ajili ya kuwajengea uwezo Waheshimiwa Madiwani an Wadau wengine kuhusu utekelezaji wa Mradi huo wenye ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi, kwani mafunzo hayo nimuongozo tosha wa elumu kwa Umma.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa