• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUWAFICHA WATOTO WENYE ULEMAVU

Posted on: June 16th, 2021

Serikali Wilayani Gairo, imepiga marufuku tabia ya baadhi ya wazazi kuwaficha watoto wenye ulemavu, kwani kwa kufanya hivyo ni kuwanyima haki zao za msingi ikiwepo kukosa elimu kulingana na uhitaji wao ns wamba tabia hiyo ni unyanyasaji wa kimaumbile.

Marufuku hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Sirieli Mchembe wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kiwilaya yamehitimishwa katika kijiji cha Mnyunhe kata ya Kibedya.

“Natoa onyo kali na iwe marufuku kuanzia sasa, mzazi au mlezi yoyote atakayebainika kumficha mtoto wenye ulemavu hatua kali zitachukuliwa dhidi yake, haiwezekani Serikali inahamasisha kila mtoto aende shule halafu wengine wanawaficha watoto wao ndani”, alisisitiza.

Alisema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaendelea kuboresha miundombinu na kuweka mazingira rafiki kwa walemavu ili kuwawezesha kunufaika na fursa ya elimu bila malipo hivyo jamii haipaswi kuwaficha na kuwa nyanyapaa watoto hao.

Akizungumzia kuhusu swala la wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa masomoni, Mhe. Mchembe aliwambia wazazi kuwa wajitokeze kwenye ofisi za kata kwa jili ya kuandikisha wanafunzi wote waliokatisha masomo kutokana na kupata mimba ili watambulike kisha uandaliwe utaratibu wa kuwarudisha mashuleni kuendelea na masomo.

Aidha aliwaasa wanafunzi wa kike kutofanya mapenzi katika umri mdogo kwani kitendo hicho kinasababisha kupata mimba zisizotarajiwa na kukatisha ndoto zao

Alifafanua “Siyo kwamba serikali imeruhusu mimba mashuleni, hapana lengo ni kuendeleza ndoto za watoto wa kike zilizokuwa zimekatika baada ya kushika ujauzito wakiwa masomoni, cha muhimu watoto wa kike mjitunze na kulinda utu wenu muweze kufikia malengo.

Aidha katika hotuba yake Mhe. Mchembe alisisitiza swala la ushurikiano kati ya wazazi wa walimu katika kufuatilia tabia na mienendo wa wanafunzi pamoja na kuchukua hatua za pamoja dhidi ya wanaume wanaowapa mimba mabinti zao badala ya kumaliza kesi za mimba vichochoroni.

Kauli mbiu ya maadhimishi ya kilele cha siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu ni Tutekeleze Agenda ya 2040 kwa Afrika inayolinda haki za Mtoto

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa