• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI: BONDIA TWAHA KIDUKU ASHIRIKI KUFANYA USAFI

Posted on: June 5th, 2023

Na/ Cosmas Mathias Njingo; GAIRO

Juni 5.2023

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini anayefanya vizuri katika anga za Kimataifa kutoka Mkoa wa Morogoro Twaha Kiduku, ameungana na Viongozi mbalimbali, Watumishi na Wananchi Wilayani Gairo, kuadhimisha SIKU ya MAZINGIRA DUNIANI kwa kushiriki shughuli za usafi wa Mazingira na ugawaji wa Miche ya Miti.
Akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Jabiri Makame, Kiduku amewataka Wakazi wa Gairo kutunza na kuhifadhi mazingira sambamba na kuhakikisha wanapanda miti kwa wingi ili kuepukana na hali ya jangwa inayoweza kusababisha ukame.
Awali Mhe. Makame aliwaambia Wananchi hao kuhakikisha kila mmoja anakuwa balozi katika shughuli za utunzaji wa mazingira kwa kufanya usafi kwenye maeneo yao, kupanda miti kwa wingi na kuhakikisha miti yote iliyopandwa inakua vizuri.
Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Msifwaki Haule, amempongeza Bondia huyo kwa kuonyesha nia thabiti ya kwenda na kuhamasisha Wananchi wa Gairo kushiriki katika shughuli za usafi na utunzaji wa mazingira pasipo kujali nafasi yake ya kuwa mtu maarufu nchini.

SIKU ya Mazingira Duniani huadhimishwa Juni 5 kila mwaka, lengo ikiwa ni kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari zitokanazo na uharibifu wa mazingira sambamba na kuhamasisha Wananchi kushiriki kwenye shughuli za usafi, upandaji wa miti na utunzaji wa vyanzo vya maji.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa