Na. Cosmas Njingo; GAIRO
Februari 23.2025
Maafisa kutoka Idara ya Habari na Elimu kwa Umma ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kwa hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika maandalizi ya zoezi la uandikishaji wapiga kura wapya pamoja na uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Pongezi hizo zilitolewa Februari 21.2025, wakati wa ziara ya maafisa hao wilayani Gairo kwa ajili ya kufuatilia hatua za maandalizi zinazoendelea kabla ya kuanza rasmi kwa zoezi hilo muhimu la kitaifa.
Wakizungumza na watendaji wa halmashauri pamoja na wadau wa uchaguzi, maafisa hao walionesha kuridhishwa na namna ambavyo Gairo imejipanga katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa kushiriki katika uboreshaji wa daftari hilo.
"Ni dhahiri kuwa Gairo imechukua hatua makini za maandalizi, ikiwemo utoaji wa elimu kwa umma, maandalizi ya miundombinu na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali. Hii inaonesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha kila mwenye sifa anashiriki kwenye zoezi hili," alisema mmoja wa maafisa wa NEC.
Kwa upande wao , viongozi wa Halmashauri ya Gairo wamesema wapo tayari kushirikiana na NEC pamoja na taasisi nyingine kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa mafanikio makubwa.Zoezi la uandikishaji na uboreshaji wa daftari linatarajiwa kuwa chachu ya kuongeza ushiriki wa wananchi kwenye uchaguzi mkuu ujao, huku NEC ikiendelea kusisitiza umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.
Sanduku la Posta: 40, GAIRO
Simu ya Mezani: +255 787730665
Simu ya Kiganjani: +255 717222572
Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz
Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa