• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

UFAFANUZI UBADHILIFU WA SH.100M MKOPO WA 10%

Posted on: April 22nd, 2023

Na Cosmas M. Njingo. GAIRO

Aprili 22.2023


UFAFANUZI TUHUMA ZA UBADHILIFU WA SH. MIL 100 ZA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU. *Naweka kumbukumbu sawa kuhusu Mil 100 za fedha za Mikopo ya Vijana, Wanawake na Watu Wenye Ulemavu.*

Nimekuwa nikiona taarifa mbalimbali zikitolewa na kuandikwa na baadhi ya Watu kwamba Kuna fedha milioni 100 za vikundi zimeliwa na Watumishi wa Halmashauri. Hili taarifa si sahihi, ni upotoshaji.

Usahihi wa taarifa ni kwamba, Timu ya Uchunguzi iliyoundwa na Mnamo Mwezi Februari 2023, ililenga kufanya Ufuatiliaji wa Mikopo ya Vikundi kupitia Mapato ya ndani. Lengo letu lilikuwa kutaka kujiridhisha kama fedha zinatolewa kwa walengwa, tija ya mikopo hiyo kwa maana uendelevu wa miradi na kuboreka kwa maisha ya wakopaji, urejeshaji wa mikopo kadhalika na uzingatiaji wa Kanuni na mwongozo wa Utoaji wa mikopo……

Kamati ilibaini changamoto kadhaa ikiwemo tabia ya baadhi ya Wananchi wanaonufaika na mikopo hiyo kutorejesha kabisa mikopo ambapo katika kipindi Cha Miaka 3 takribani kiasi Cha shilingi mil 100 hazijarejeshwa na Vikundi), baadhi ya vikundi kugawana mikopo bila kufanya miradi iliyokusudiwa na Vikundi kusambaratika, kutolewa kwa mikopo kwa Vikundi visivyokidhi vigezo, tija ndogo ya mikopo hiyo na baadhi ya mikopo kutolewa bila kuzingatia Mwongozo……

Kufautia dosari hizo, imeelekezwa kwamba;-

*Moja, ndani ya siku 14 Halmashauri ije na Mpango wa kurejesha fedha kutoka kwenye vikundi kwa maana ya Mkakati wa namna ya kuzifuatilia fedha hizo kutoka kwa waliokopeswa, siyo Halmashauri irejeshe fedha ndani ya siku 14 kama baadhi ya Watu wanavyopotosha.*

*Pili, TAKUKURU wanaendelea na ufuatiliaji. Kama Kuna Mtumishi au Mwananchi amehusika katika jambo lolote la Rushwa hatua za kisheria zitachukuliwa.*

Hivyo, fedha Shilingi mil 100 zilizozungumzwa ni fedha za Mikopo ambazo Vikundi havijarejesha kwa Halmashauri.

Ikumbukwe kwamba, baadhi ya wakopaji ni ndugu zetu, wananchi wenzetu, Vijana wenzetu hivyo na wao wanahusika, na niwaombe tuwajulishe kwamba fedha hizo lazima zirejeshwe ili wananchi wengine wanufaike pindi Serikali itakapotoa utaratibu mpya. Hatutasita kuchukua hatua kwa wale waliochukua fedha za Halmashauri bila kurejesha.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa