• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

UJENZI WA CHUO CHA VETA GAIRO WAANZA RASMI, TSH.1.4 BILIONI KUTUMIKA AWAMU YA KWANZA

Posted on: June 9th, 2023

Na. Cosmas Mathias Njingo;GAIRO

Juni 9.2023

TZS.1,400,000,000 (1.4 Bil) KUTEKELEZA AWAMU YA KWANZA YA UJENZI WA CHUO CHA MAFUNZO YA UFUNDI STADI GAIRO

#Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Makame amezindua rasmi utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Chuo Cha Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Wilaya ya Gairo, ambao utasaidia kuongeza fursa kwa vijana kupata ujuzi wa kujiajiri wao wenyewe baada ya kuhitimu masomo.

Tukio hilo la Uzinduzi limefanyika Mei.7.2023 kwenye Kijiji Cha Msingisi Kata ya Msingisi Wilayani Gairo ambapo chuo hicho kitajengwa.

Kwa mujibu wa Mthibiti Mkuu wa Ubora wa Elimu Wilayani Gairo Bi. Tatu Samizi, hadi kukamilika kwa awamu ya kwanza ya Ujenzi wa Majengo tisa, jumla ya Shingi Bilioni Moja, na milioni mianne zitatumika , na kufafanua kuwa tayari kiasi Cha shilingi 228 Milioni kimeshawekwa kwenye akaunti kwa ajili ya kuanza utekelezaji.

"Mhe. Mgeni Rasmi awamu ya kwanza ya Mradi huu inajumuisha Ujenzi wa Majengo 9, likiwepo Jengo la Utawala, Jengo la Mlizi, Jengo la Kuzalishia Umeme (power house), Utawala, Nyumba ya Mkuu wa Chuo, Ofisi, Jengo la vyumba 03 vya madarasa, na kiasi cha shilingi Bilioni Moja na milioni mianne zitatumika katika Ujenzi wa Majengo hayo tisa". Alifafanua Bi. Samizi.

Akihutubia Wakazi wa eneo hilo Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Makame alisema kwa mwaka huu wa 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imepokea fedha zaidi ya Bilioni mbili kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya Elimu ya Awali na Msingi ili kuongeza utoaji wa huduma na kuweka Mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia, hivyo uwepo wa chuo hicho cha VETA Wilayani Gairo ni fursa ya kipekee kwa Wakazi wa Gairo.

"Mhe. Rais ameleta Fedha nyingi sana kwenye Wilaya yetu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali sekta ya Elimu, afya, barabara na maji. Na sasa tumepokea fedha shilingi Bilioni Moja nukata nne za ujenzi wa Chuo cha VETA, hii ni fursa kwa vijana wetu kupata ujuzi utakao wasaidia kujiajiri". Alisema Mhe. Makame.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo Ndg. Danistani Mwendi alisema maendeleo ya kasi yanayotokea Wilayani humo, ni juhudi kubwa za Mhe. Shabiby Mbunge wa Jimbo la Gairo ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kupigania upatikanaji wa Fedha kutoka serikali kuu.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa