• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VIJANA WAWEZESHWA MAFUZO STADI YA UTENGENEZAJI VIHENGE VYA KUHIFADHIA MAZAO KUZUIA SUMUKUVU

Posted on: August 16th, 2023

 Na. Cosmas Mathias Njingo. GAIRO

Agosti 16.2023.Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kushirkiana na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi Veta imebuni mikakati ya kukabiliana na tatizo la Sumukuvu katika mazao kwa kutoa mafunzo ya utengenezaji wa Vihenge vya chuma kwa ajili uya kuhifadhia mazao pasipo matumizi ya kemikali.

Jumla ya vijana 17 kutoka Wilayani Gairo walishiriki na kuhitmu mafunzo hayo ya mwezi mmoja yaliyoendeshwa na chuo hicho, yakilenga kuondoa changamoto ya kuwepo kwa sumukuvu katika nafaka aina ya mahindi na karaka kutokana na njia mbovu za uhifadhi wa mazao hayo.

Akizungumza mbele Wajumbe wa Kikao cha Kawaida cha Baraza la Waheshimiwa Madiwani, wakati wa kukabidhiwa vifaa na vitendea kazi kwa ajili ya kutengenezea vihenge hivyo vya chuma, Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka Wizara ya Kilimo, aliwaeleza Waheshimiwa Madiwani kuwa; vijana waliopata mafunzo hayo wanatoka katika kata mbalimbali za Wilaya ya Gairo.

Alisema lengo la Serikali ni kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara ya sumukuvu kwa binadamu, kwani endapo itatumika kwa wingi inaweza kusababisha vifo kwa binadamu na mifugo, hivyo Serikali imekuja na mpango huo ili kuwezesha wakulima kuhifadhi mazao yao katika hali salama zaidi.

“Sumukuvu ikitumika kwa kiwango kikubwa, sote tunajua kuwa madhara yake husababisha vifo kwa watumiaji wa mazao yaliyoathiriwa na ukungu aina ya kuvu ambao hubadilika na kuwa sumu, na endapo sumukuvu italiwa kwa kiwango kidogo inasababisha saratani katika mwili wa Binadamu”. Alibainisha Mratibu huyo.

Mratibu huyo kutoka Wizara ya Kilimo akafafanua kuwa baada ya kuhitimu mafunzo hayo, Serikali imetoa bure vitendea kazi maalum kwa vijana hao kwa ajili ya kuanza rasmi mradi wa utengenezaji wa vihenga vya chuma.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Rahel Nyangasi; akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Wahe. Madiwani, aliwapongeza na kuwaasa vijana hao 17 kuvitumia kwa manufaa ya umma na kuvitunza kwa uangalifu ili juhudi za serikali za kupambana na tatizo la sumukuvu zisipote bure.

“Niwapongeze Vijana wote 17 waliohitimu mafunzo, pia ninaishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mama yetu Mhe. Rais Dakta Samia, kwa kuendelea kuipendelea Gairo kupitia miradi mbalimbali ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi. Rai yangu kwenu; vifaa hivi mkavitunze na kuvitumia kwa manufaa mapana ya kukabiliana na changamoto ya Sumukuvu katika Wilaya yetu ili kuwezesha Wakulima kupata vihenge bora vya chuma vya kuhifadhia nafaka”. Mwenyekiti Nyangasi aliwaasa.

Vijana hao walikabidhiwa jumla ya vifaa tisa kila mmoja ikiwepo Mashine ya kuchomelea, mashine ya kutobolea vyuma, msumeno, evider, Kamba ya kupimia (tape measure), try square pamoja na punch, hivi vyote vinamuwezesha fundi kukamilsha kazi ya utengenezaji wa vihenge bila usumbufu wa aina yoyote.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa