• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Posted on: February 24th, 2025

Na. Cosmas Mathias Njingo; GAIRO 

Februari 24.2025

Maafisa Waandikishaji Wasaidizi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ngazi ya jimbo, Wilaya ya Gairo,  wamekutana na viongozi wa dini katika kikao maalum kilicholenga kujadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mhe. Rais, Waheshimiwa Wabunge na Madiwani.

Mkutano huo ambao umefanyika katika ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri Februari 21.2025 umelenga kuhakikisha viongozi wa dini ambao ni wadau muhimu katika jamii, wanashirikiana na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwahamasisha waumini wao kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uboreshaji wa daftari hilo muhimu kwa hatima ya ushiriki wa kidemokrasia.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Afisa Mwandikishaji Msaidizi wa Jimbo Bi. Jane Sanga, amesisitiza kuwa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ni zoezi la msingi linalowapa wananchi fursa ya kikatiba ya kushiriki katika kuwapata viongozi wa ngazi mbalimbali kwa njia ya kidemokrasia.

“Tunatambua nafasi kubwa na ushawishi wa viongozi wa dini katika jamii. Kupitia mafundisho na mikusanyiko yao ya kila wiki, wanaweza kufikisha ujumbe wa kuhamasisha uandikishaji wa wapiga kura wapya na wale wanaopaswa kusahihisha taarifa zao,” alisema Bi. Sanga.

Kwa upande wao, viongozi hao wa dini walionesha utayari wao kushirikiana na NEC katika kufanikisha zoezi hilo, wakisisitiza kuwa ushiriki wa waumini wao katika uchaguzi unategemea moja kwa moja na uelewa wao wa umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.

Mwenyekiti wa mwenza wa Jukwaa la Amani dini mbalimbali, Mchungaji Canon Mmbelwa, alisema wanatambua umuhimu wao katika kuhimiza Waumini wa di ni zote kushiriki katika zoezi la kujiandikisha ili kupata sifa za kupiga kura, hivyo watatumia majukwaa ya ibada kutoa elimu hiyo.

“Tutatumia majukwaa yetu ya ibada kuwaelimisha waumini juu ya wajibu wao wa kikatiba na kiraia. Tunatambua kuwa kushiriki uchaguzi ni sehemu ya kuchangia maendeleo ya nchi.”

Aidha, mkutano huo ulijadili changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza katika mchakato huo, ikiwemo upotoshaji wa taarifa mitandaoni, mwamko mdogo wa baadhi ya makundi ya jamii, na hitaji la ushirikiano baina ya wadau wote katika kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia wananchi.

Zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linatarajiwa kuanza tarehe 1na kukamilika tarehe 7 Machi 2025 katika vituo 94 vya kata 18 za Halmashuri ya Wilaya ya Gairo, huku Tume ikisisitiza umuhimu wa kila mwananchi mwenye sifa kujitokeza ili aweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa