• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VIONGOZI WAHIMIZE WAKULIMA KUJISAJILI

Posted on: October 2nd, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Oktoba 2, 2022.

 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Abubakar Mwassa, amewataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Wataalam wa Kilimo wa Mkoa huo, kuhakikisha wanahimiza wakulima kujiandikisha katika daftari la wakulima, ili kunufaika na punguzo la bei ya mbolea za ruzuku.

Ametoa wito huo Oktoba Mosi 2022, katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Kilimo Marathoni, kilichofanyika kwenye viwanja vya Jamhuri Manispaa ya Morogoro, ambapo alisema ni wajibu wa viongozi wote kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha na kuhimiza wakulima kujiandikishwa kwenye daftari hilo ili kuiwezesha Serikali kutambua idadi yao, hali ambayo itarahisisha kuwahudumia.

Mhe. Fatma Mwassa, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akifungua kikao cha Wadau wa Kilimo kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Morena Manispaa ya Morogoro.

“Jambo kubwa kwa sasa tuhimize wakulima kujisajili, kwani kupitia zoezi hili wakulima watapata fursa mbalimbali ikiwepo kunufaika na punguzo la bei za bembejeo za kilimo, kwa kuwa mama yetu Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha mapenzi makubwa kwa wakulima wetu kwa kuwashusia bei ya mbolea na Mbegu kutokana na ruzuku aliyoilekeza kwa Wakulima”. Alisisitiza Mhe. Mwassa.

Mkuu huyo wa Mkoa akasme kuwa, Mkoa wa Morogoro una Wakulima wasiopungua 470,000 (laki nne na elfu sabini), lakini wakulima waliojiandikisha ni asilimia 33 tu ya wakulima wote, hivyo ni vyema Wataalam wa Kilimo kwa ngazi zote kuhakikisha wanawafikia wakulima wote na kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa kusajiliwa katika daftari la kudumu la Wakulima, ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo iliyokusudia katika kuhakikisha kilimo kinakuwa na tija nchini.

Baadi ya wadau walioshikiri mbio za umbali mbali mbali baada ya kukabidhiwa tuzo zao na Mhe. Fatma Mwassa, katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa

“Mkoa wetu unakadiriwa kuwa na Wakulima laki nne na sabini elfu, lakini hadi sasa ni asilimia 33 tu ya wakulima wote walioandishwa. Bado hali ya uandikishaji hairidhishi, hivyo nendeni mkawahimize wakulima wetu wapata kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya Wakulima ili kutimiza malengo ya Serikali ya kuwahudumia wakulika wote kwa lengo la kukifanya kilimo kuwa na tija kwa mkulima mmoja mmoja na Taifa kwa kwa ujumla”, Alielekeza Mkuu wa Mkoa Mhe. Mwassa.

Hitimisho la Wiki ya Mbio za Kilimo (Kilimo Marathon) Mkoa wa Morogoro liilitangu na kikao kazi cha wadau wa kilimo kilimo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Morena Hotel chini ya Mhe. Mwassa kujadili changamoto na mikakati mbalimbali ya kuinua sekta ya kilimo pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Baadhi ya wahiriki wa Kilimo Marathoni wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Fatma Mwassa, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro

Pamoja na shughuli nyingine kilimo marathon iliambatana na maonesho ya bidaa mbalimbali za mazao ya kilimo, pembejeo na mbolea za ruzuku pamoja na teknolijia mbalimbali za kisas zinazotumika katika mapinduzi ya kisekta ili kuongeza tija kwenye shughuli za kilimo na ufugaji.

Washiriki wa maoneho ya Kilimo Marathoni kutoka kikundi cha Chinyankala saa

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa