• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Posted on: February 21st, 2025

Tanzania – Mei 2025

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jimbo la Gairo, imevihimiza vyama vya siasa nchini kuhakikisha vinahamasisha wanachama na wafuasi wao kujitokeza kwa wingi kushiriki katika awamu ya kwanza ya uandikishaji na uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Wito huo umetolewa na Afisa Mwandikishaji Msaidizi wa Tume katika Jimbo la gairo Bi Jane Sanga, katika kikao kazi na viongozi wa vyama vya Siasa Wilaya ya Gairo, kilichoketi Februari 21. 2025, kuelekea uzinduzi rasmi wa zoezi hilo unaotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe  hadi 7 machi 12025 katika maeneo mbalimbali ya nchi, ambapo wananchi wanahamasishwa kujisajili kwa mara ya kwanza au kuboresha taarifa zao zilizopo katika daftari hilo.

Akizungumza na Viongozi hao, Bi. Jane Sanga alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vyama vya siasa katika mchakato huo kwa kuwa wao ni wadau wakuu wa uchaguzi na wana nafasi kubwa katika kuhakikisha wananchi wanatimiza haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.

"Vyama vya siasa vina jukumu la msingi kuhakikisha wanachama wao wanapata elimu ya uchaguzi, wanajitokeza katika vituo vya kujiandikisha na kuhakikisha taarifa zao ziko sahihi. Hili ni zoezi la kitaifa na la kidemokrasia ambalo linahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Tume, vyama vya siasa na wananchi," alisema msemaji huyo.

Aidha, NEC imewataka viongozi wa vyama kuwaelimisha wanachama kuhusu umuhimu wa ushiriki katika uandikishaji huo kama njia ya kujiandaa kushiriki kikamilifu kwenye chaguzi zijazo, huku ikikumbusha kuwa daftari hilo ndilo linalotumika rasmi kwenye uchaguzi wowote wa kitaifa au wa serikali za mitaa.

Wananchi wote wanaostahili kuandikishwa, wakiwemo vijana waliotimiza umri wa miaka 18 au wanaotarajia kutimiza umri huo kabla ya uchaguzi, wametakiwa kujitokeza na kufika kwenye vituo vilivyotengwa kwa ajili ya huduma hiyo.

Uandikishaji na uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ni hatua muhimu inayochangia uhalali na uwazi wa mchakato wa uchaguzi nchini, na hivyo ushiriki wa kila mwananchi na taasisi husika unahitajika kwa mafanikio ya demokrasia ya Tanzania.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa