• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUCHAMBUA, KUANDIKA, KUTOA TAARIFA SAHIHI KWA UMMA

Posted on: June 18th, 2024

Na. Cosmas Mathias Njingo. DAR ES  SALAAM

Juni 19.2024

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewaasa Waandishi wa Habari na Wadau wa Sekta ya Habari nchini kutumia taaluma zao vizuri kwa ufanya uchambuzi wa habari, kutoa taarifa sahihi kwa umma na kuisema vizuri Serikali badala ya kuandika mapungufu pekee ya Serikali.

Ametoa wito huo Juni 18.2024 akifungua kongamano la Pili la Maendeleo ya Sekta ya Habari katika ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam, ambalo Wadau wa sekata ya Habari watakutana kwa siku mbili hadi Juni 19.2024 kujadili mafanikio ya sekta hiyo, changamoto na mikakati ya kuboresha utoaji wa huduma za habari na mawasiliano Nchini.

“Nitoe rai yangu kwa Waandishi wa habari Nchini kote, mjitahidi kuandika mazuri na kuisemea vizuri Nchi yetu ya Tanzania, badala ya kuandika habari za kuichafua Serikali. Ninyi ni watu muhimu sana wa kutangaza yaliyomema ambayo yanaleta tija kwa Wananachi”. Alisema Mhe. Rais Samia.

Samia aliwaambia Washiriki wa Kongamano hilo kutumia kalamu zao vizuri kuandika habari chanya kwa jamii pamoja na kukanusha taarifa mbalimbali za upotoshaji zinazosambazwa na baadhi ya Waandishi wasio zingatia maadili ya Taaluma hiyo, huku wengine wakiitukana Serikali katika uso wa dunia, hali ambayo alisema inalenga kuzua taharuki na kuharibu taswira njema ya Nchi kwenye nyanja za Kimataifa.

“Tumieni vizuri kalamu zenu kuhabarisha Umma yale mema ambayo Serikali inayafanya, tunamiradi mingi ya maendeleo inatekelezwa huko kwenye ngazi za Halmashauri, wajulisheini Wananchi kuhusu miradi hiyo. Lakini cha ajabu ukiingia huko kwenye mitandao ya kijamii unakutana na matusi tu ya kuichafua Serikali”. Alisikitishwa.

Aidha Mhe. Rais Samia aliwataka Wanahabari hao kufanya uchambuzi wa kina wa taarifa kabla ya kuzirusha kwa jamii ili kupata usahihi wa kile wanachokusudia kuuhabarisha Umma, na hiyo itasaidia Wanachi kupata taarifa za kina, badala ya kusikia jambo na kulirusha bila kufanya uchambuzi wa kutosha.

Kongamano hilo la Maendeleo ya Sekta ya Habari limehuduhriwa na Washiriki mbalimbali kutoka Wizara na Taasisi za Umma, Binafsi, Viongozi wa Vyombo vya Habari, Waandishi wa Habari, Maafisa Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali na Wadau wengine, ambapo litafuatiwa na Kikaoa kazi cha 19 cha Maafisa Habari wa Serikali kuanzia Juni 20 hadi 22.2022

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHIRIKIANA NA NEC KUHAMASISHA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 24, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAIPONGEZA HALMASHAURI KWA MAANDALIZI MAZURI

    February 23, 2025
  • VYAMA VYA SISA VYAHIMIZWA KUHAMASISHA WANACHAMA WAO KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA AWAMU YA KWANZA YA UANDIKISHAJI, UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 21, 2025
  • MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUIWEKA WILAYA YA GAIRO KWENYE RAMANI YA UZALISHAJI WA PARACHICHI NCHINI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa