• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WADAU WA ELIMU GAIRO WAKUSANYA SH.38 MILIONI KATIKA HARAMBEE YA KUTUNISHA MFUKO WA ELIMU

Posted on: January 14th, 2022

Wilaya ya Gairo imezindua mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia sekta ya Elimu ikiwa ni kampeni ya kuboresha miundombinu chakavu mashuleni sambamba na kupambana na utoro uliokithiri na mimba za utotoni ambavyo vinatajwa kuchangia udumavu wa elimu kwa shule za msingi.

Uzinduzi huo umefanyika Januari 14.2022 katika Ukumbi wa Nazareth kata ya Magoweko chini ya Mhe. Jabiri Omari Makame, Mkuu wa Wilaya ya Gairo, umeenda sambamba na harambee ya kuchangia fedha za kutunisha Mfuko wa Elimu kwa lengo la kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikumba sekta ya elimu.

“Jumla ya Shilingi 38,630,000 zimepatikana kwa muda mfupi sana. Nianze kwa kuwashukuru wadau wote mlio onyesha nia ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya wamau ya sita za kuhakikisha elimu inapewa kipaumbele ili vijana wetu wasome katika mazingira safi na rafiki”, alisema Mkuu huyo wa Wilaya

Na kuongeza kuwa “Ikiwa ni mara ya kwanza kwa Wilaya yetu kuendesha zoezi hili, nina kila sababu ya kutembea kifua mbele kwa fedha hizi kwa kukubali kwenu kuniunga mkono katika kampeni hii muhimu ya kusaidia kutatua changamoto zinazo wakabili watoto wetu mashuleni”, alifafanua.

Akitangaza kiasi kilichopatikana katika changizo hilo Mhe. Makame aliwapongeza Wadau hao kwa kuonyesha nia ya dhati kunusuru sekta ya elimu, kwani jukumu la kuinua kiwango cha elimu na kuongeza ufaulu mashuleni ni la jamii nzima ambapo aliwaomba wadau hao kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hasan katika hushughulikia kero za elimu.

Akasema kwamba “ Swala la ujenzo wa elimu bora siyo swala la walimu peke yao bali jamii nzima inawajibika kuhakikisha inashiriki katika kuboresha hali ya taaluma kuanzia nyumbani hadi mashuleni ili kutokomeza utoro, mimba za utotoni  na utendaji kazi mbovu wa walimu kwa kuhakikisha miundombinu yote ya elimu ni safi, salana na rafiki”.

Uchakavu wa miundombinu, ubovu wa majengo ya shule, upungufu wa madarasa, madawati, viti na meza pamoja na upungufu wa walimu ni kati ya sababu zinazotajwa kuwa kikwazo kikubwa za kupunguza ari ya kujifunza na kufundisha na kwamba zimechochea matokeo mabovu katika mitihani ya kujipima na Taifa.

Kiasi cha Shilingi milioni 38,630,000 zilipatikana wakati wa zoezi la harambee ya kutunisha mfuko huo ambapo kati ya hizo Shilingi 40,000 ni fedha tasilimu na ahadi shilingi 38,590,000 huku wakala wa misitu gairo (TFS) pamoja na Mhifadhi wa Milima ya Ukaguru walichangia kiasi cha shilingi 20,000,000.

Kuanzishwa kwa Mfuko kunalenga kusaidia katika kutatua changamoto mbalimbali zinazo ikabili sekta ya Elimu ambazo zinatajwa kuwa kikwazo kikubwa cha kuzorotesha ustawi wa elimu ngazi ya Msingi na Sekondari.

Baadhi ya Wadau wakitoa maoni yao kuhusu kuimarisha Sekta ya elimu walishauri fedha zilizopatikana kupitia harambee hiyo zielekezewe kwenye ujenzi wa shule ya sekondari ya Wasichana yenye mchepuo wa Sayansi ili kuzalisha wanasayansi wengi wanawake.

“Mimi ninashauri mfuko huu ukishaa anzishwa, fedha zinakazo patikana Uongozi wa Wilaya uone namna ya kuwekeza kwenye ujenzi wa shule ya wasichana ya sayansi”, alishauri mmoja wa wadau hao ambae jina lake halikuweza kupatikana.

Aidha kupitia harambee hiyo Wakala wa Misitu (TFS) Gairo kwa kushirikiana na Mhifadhi Milima ya Ukaguru walitoa jumla ya Shilingi 20,000,000 ambazo walisema zitaelekezwa kwenye kuboresha miundombinu chakavu shule ya msingi mandenge.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa