• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WADAU WA KILIMO MOROGORO WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA KILIMO BORA YA CHENYE TIJA.

Posted on: October 3rd, 2022

Cosmas Mathias Njingo; 

MOROGORO.

Oktoba 3, 2022.

Wadau wa Kilimo Mko wa Morogoro Wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Fatma Abubakar Mwassa wamekutana katika kongamano la wadau wa Sekta hiyo kujadili changamoto na mikakati mbalimbali ya kilimo chenye tija bila kuleta athari za mazingira na kijamii.

Kongamano hilo la siku 1 limefanyika Septemba 28.2022 katika ukumbi wa Hoteli ya Morena iliyopo Msamvu Manisapaa ya Morogoro, ambapo wadau kutoka taasisi za Umma na Binafsi zinazojihusisha na tafiti na elimu ya kilimo walikutana pamoja na Wataala wa Idara za kilimo kutoka Halmashauri za Mkoa huo.

Akifungua kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Mwassa, alisema kongamano hilo ni muhimu kwa mustakabali wa afya ya sekta ya kilimo, kwani kunawawezesha wadau kuona fursa za kiuchumi zilizopo na kuzitumia, badala ya kutumia muda mwingi kulalamika au kutatua miogogoro.

“Ili Wananachi wa Mkoa wa Morogoro walime kwa tija, tunahitaji kufanya mabadiliko (transformation) ya kifikra, tunahitaji mabadiliko ya namna tunavyotenda mambo na mabadiliko ya kimfumo, na inapobidi mabadiliko ya kiuongozi. Hivyo kupitia kongamano hili ni imani yangu kuwa yale tutakayojadili yataleta changamoto katika kutumia fursa zilizopo ndani ya mkoa wetu, ili kilimo kiwe na tija kwa faida ya mtu mmoja mmoja, mkoa na Taifa kwa ujumla”. Alisema Mhe. Mwassa.

Alisema Mkoa wa morogoro una ardhi yenye rutuba ya kutosha na hali ya hewa nzuri inayostawisha mazao mengi, mvua za wasta kati ya 600mm hadi 800mm, lakini pamoja na hali hiyo bado sekta ya kilimo haifanyi vizuri.

Akizungumzia kuhusu migogoro ya Ardhi, Mhe. Mwassa alibainisha kuwa Morogoro ni miongoni mwa mikoa 5 nchini inayokabiliwa na migogoro sugu ya Ardhi, ikiwepo kati ya kijiji na kijiji, wakulima na wafugaji na katika ya koo flani na koo nyingine. Kwa kuongeza kuwa Watendaji wa Serikali wameshindwa kusimamia vizuri juu ya matumizi ya ardhi iliyopo.

“Bado tunaeneo kubwa sana ikilinganishwa na idadi ya watu waliopo mkoa wa Morogoro. Hivyo nisingependa kuona ongezeko la migogoro ya ardhi kati ya Wakulima na Wafugaji kama tuliyonayo hivi sasa.

Mkoa wa Morogoro ni mkoa wa pili Tanzania kwa Ukubwa, ukiwa na hekta za mraba 73,039,000. Hadi kufikia mwaka 2012 Morogoro ilikadiriwa kuwa na wakaazi 2,827,281 (milioni mbili laki nane thamanini na saba elfu miambili themanini na moja), kwa mujibu wa sense ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 kukiwa kuna ongezeko la asilimia 3.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa