• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAENDESHA BAISKELI NCHI ZA JUMUIA YA EAC KUPEPERUSHA BENDERA YA SENSA

Posted on: August 20th, 2022

GAIRO, MOROGORO.

Na. Cosmas Mathias Njingo.

Wakati Tanzania ikiendelea na maandalizi mbalimbali ya kungia katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linalotarajiwa kufanyika tarehe 23 Agosti 20, Timu ya Vijana waendesha Baiskeli wapatao 35 kutoka Mataifa yanayounda umoja wa Jumuiya ya Afrika mashariki wameamua kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupeperusha Bendera ya Sensa kwa lengo la kutangaza ujumbe wa zoezi hilo na kuhamasisha Watanzania kushiriki kuhesabiwa kupitia matembezi ya basikeli kuzunguka Nchi zailizopo katika ukansa wa Afirika Mashariki.

(Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame (kulia), akikabidi Bendera ya Sensa kwa Kiongozi wa waendesha Baiskeli kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki)

Agosti 20.2022 Wilaya ya Gairo ilipokea Timu ya Vijana hao wakitokea Mji wa Mombasa Nchini Kenya katika ziara yao ya kuhamsisha Viongozi wa Mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kudumisha Amani, Umoja, Mshikamano, Utunzaji wa Mazingira na upandaji wa Miti, wakipita kwenye Nchi zote za EAU.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame aliwakabidhi vijana hao Bendera ya Sensa na kuwataka kuendelea kutangaza ujumbe huo kwa kila mkoa wa Tanzania ambao wamepanga kupita kuelekea Nchi za Congo, Rwanda, Burudi, Sudani Kusini na Uganda kabla ya kuhitimisha matembezi hayo katika Jiji la Nairobi Nchini Kenya ili kuongeza hamasa na uelewa wa pamoja kwa wananchi watambue umuhimu wa kuhesabiwa.

(Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame akiongoza matembezi ya Waendesha Baiskeli kutoka Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki kuhamasisha amani, umoja, utunzaji wa mazingira na kueneza ujumbe wa Sensa ya watu na Makazi)

Mmoja wa Viongozi wa vijana hao waendesha Basikeli kutoka nchi zipatazo Saba (7) za Kumuiya ya Afrilka mashariki alisema Serikali haiwezi kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo ikiwa haitambui idadi ya watu wake, na kusisitiza kuwa ni muhimu kila mtanzania kujitokeza kuhesabiwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu na kuharakisha maendeleo.

“Mipango ndiyo inayo endesha Nchi, inasaidia Serikali kubaini mahali flani kuwa watu kiasi Fulani na wanahitaji huduma flani, mfano Shule, mahitaji ya vituo vya kutolea huduma za afya, miundombinu ya barabara na uboreshaji wa huduma nyingine za kijamii.” alieleza kiongozi huyo.

(Waendesha Baiskeli kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki) 

Naye Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri Omari Makame, amewapongeza vijana hao kwa kazu nzuri ya kizalendo kwa kujitolea kutembea kwa Baiskeli kuzunguka katika Nchi zote za Jumuiya ya EAC kwa lengo la kutangaza Umoja na mshikamano, ambapo aliwataka kutumia fursa hiyo kutangaza ujumbe wa Sensa kwa Watanzania katika mikoa yote ya Tanzania Watakayopita.

“Ninawapongeza kwa kazi nzuri ya kizalendo, mmeonyesha ujasiri mkubwa wa kutembea kwa Baiskeli mkizunguka na ujumbe wa kueneza Amani, Mshikamano na Umoja. Nami ninawaomba kupitia matembezi haya mtusaidie kupeperusha Bendera yetu yenye ujumbe wa Sensa katika kila mkoa mtakao fika msisahau kuhamasisha kukushu zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ili kila Mtanzania atambue umuhimu wa kuhesabiwa ifikapo Agosti 23.2022”. alisema Mhe. Makame.

Matangazo ya Kawaida

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari za Gairo December 16, 2022
  • SOMA TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI May 25, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUZOA TAKA, KUFANYA USAFI NA KUKUSANYA USHURU WA USAFI June 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHONGOLO ATIMIZA AHADI YAKE

    February 16, 2023
  • DCC YAPITISHA BAJETI YA SH.1.7 BILIONI

    February 15, 2023
  • WAKANDARASI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UFANISI

    February 14, 2023
  • RAIS SAMIA AWATAKA VIJANA KUWA NA ARI YA KULITUMIKIA TAIFA

    February 11, 2023
  • Tazama zote

Video

MWANASHERIA MSOMI AAMUA KUUZA JUISI MITAANI
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA SITA 2022 GAIRO SEKONDARI
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255232935454

    Simu ya Kiganjani: +255 767498981

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa