• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAKAZI WA MKOA WA MOROGORO WANAKABILIWA NA UKOSEFU WA ELIMU YA FURSA KATIKA SEKTA YA KILIMO

Posted on: September 30th, 2022

Na. Cosmas Mathiasn Njingo

Morogoro.

Septemba 30.2022

Pamoja na kuwepo kwa ardhi yenye rutuba nzuri zaidi ya hekari milioni mbili inayofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali ya biashara katika mkoa wa morogoro, ni asilimia 40 tu ya eneo la ardhi linalotumika kwa shughuli za kilimo, huku asilimia 60 zikibaki mapori tupu, hali ambayo inatajwa kuchangia uzalishaji usio na tija.

Dakta Chagoba Zaidi Mkangwa, Mtafiti Mstaafu kutoka Asasi ya Kiraia inayojihusisha na Utafiti, Ushauri na Taarifa za Kilimo, iliyopo Mkoani Morogoro, alisema pamoja na kuwepo na eneo kubwa la ardhi inayofaa kwa kilimo na ufugaji, ni sehemu ndogo tu ya ardhi inayotumika kwa ajili ya shughuli hizo, huku sehemu kubwa ya ardhi hiyo ikibaki bila matumizi yoyote, na kwamba Wakulima wengi hawajatambu namna ya kutumia fursa zilizopo.

“Tunaeneo kubwa sana la ardhi lenye ukubwa zaidi ya Hekari milioni mbili, lakini ni asilimia 40 tu inayotumika kwa ajili ya shughuli za kilimo, wakati asilimia 60 ya ardhi yote inabaki wazi. Lakini changamoto kubwa ni ukosefu wa elimu juu ya matumizi ya fursa zilizopo katika sekta ya Kilimo”. Alisema Dakta Mkamgwa.

Dakta Mkangwa, akasema kuwa Mkoa wa Morogoro una fursa nyingi za kwekeza katika sekta ya Kilimo, lakini wakazi wake wanakabiliwa na changamoto ukosefu wa elimu na taarifa za kutosha kuhusu namna ya kutumia fursa hizo ili kujikita katika kilimo chenye tija na kuondokana na hali ya umaskini.

“Pamoja na changanmoto mbalimbali, Wakazi wa Mkoa wa Morogor hawajui fursa nyingi zilizopo katika sekta ya kilimo, hii inasababisha kuwa na kilimo cha mazoea na matokea yake kupata mazao yasiyo na tija kwani chini ya asilimia 40 au chini ya hapo ya kiwango kinachotakiwa kuzalishwa”. Alisfafanua Daktari huyo.

Mkangwa akaeleza changamoto nyingine zinazosababisha kuzalisha mazao hafifu ni ukosefu wa elimu ya mbinu bora za kilimo, migogoro kati ya wakulima na wafugaji pamoja na uharibifu wa nazingira ikiwepo vyanzo vya maji na uchomaji wato misitu.

 

Aidha Dakta Mkangwa amewataka Wananchi hususani wakulima wa Mkoa wa Morogoro kutumia fursa hizo kwa kuhakikisha wanazingatia na kufuafuata kanuni za kilimo bora ili kuzalisha mazao yenye tija kwa lengo la kujikwamu kiuchumi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa