• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAMSHUKURU RAIS KUBORESHA SEKTA YA ELIMU KATA YA LESHATA

Posted on: July 1st, 2023

Na. Cosmas mathias Njingo, GAIRO

Julai 1.2023


Wananchi wa Kijiji cha Leshata,Kata ya Leshata Wilayani Gairo Mkoa wa Morogoro, wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dakta Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaboreshea miundombinu Sekta ya Elimu ya Awali na Msingi baada ya Kijiji hicho kupokea Fedha Kiasi cha Sh.155,800,000 kupitia akaunti ya Shule, za utekelezaji wa Ujenzi wa Nyumba ya Walimu (pacha mbili), Madarasa mawili ya Mfano Elimu Awali na matundu Sita ya Vyoo.

Wametoa shukrani hizo Juni 30 2023 wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Sharifa Nabalang'anya ya kukagua Maendeleo ya utekelezaji wa Ujenzi wa Miradi hiyo kwa Fedha za BOOST.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Ndg. Method Exavery amesema Ujenzi wa miundombinu hiyo utasaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa Madarasa na madawati uliyodumu kwa miaka mingi hali amabyo ilisababisha kuwepo kwa mazingira magumu ya ufundishaji na kujifunzia.

Naye mmoja wa Wananchi wa Kijiji hicho Bi. Aziza Saidi Kidile, amempongeza Mhe. Rais Samia kwa kutambua changamoto za ukosefu wa nyumba kwa Walimu na kuamua kuwekeza Fedha nyingi za Ujenzi wa Nyumba bora, za kisasa ambazo zitarejesha heshima na hadi ya Walimu kwa kuwa wengi wao wamepanga mitaani kwenye nyumba ambazo hazikidhi hadhi ya Mtumishi wa Umma.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Nabalang'anya amezitaka Kamati za usimamizi wa Ujenzi wa shule zote, Walimu na Mafundi wanaotekeleza Miradi hiyo kuhakikisha majengo yote yanakuwa katika Ubora mashubuti ili thamani ya fedha iendane sanjari na uimara, Ubora na unadhifu wa miundombinu hiyo.

Aidha Mkurugenzi huyo amewaagiza Walimu Wakuu wa Shule ambazo hazina changamoto ya upatikanaji wa maji kuhakikisha wanapanda miti ya kutosha kuzunguka maeneo ya Shule hizo ili kuweka mazingira kwenye hali nadhifu pamoja na kupunguza upepo mkali unaweza kusababisha madhara ikiwepo kung'oa paa za majengo hayo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa