• Mawasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
GAIRO DISTRICT COUNCIL
GAIRO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Authorities Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dira
    • Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni za Halmashauri
      • Seksheni ya Rasilimali Watu
      • Seksheni ya Utawala
    • Divisheni ya Mipango na Ufuatiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Baraza la Madiwani
  • Miradi
    • Miradi ya Maendeleo
      • Sekta ya Elimu Msingi
        • Miradi Mipya
        • Miradi iliyokamilika
      • Sekta ya Elimu Sekondari
      • Sekta ya Afya
      • Sekta ya Barabara/Miundombinu
      • Sekta ya Maji
  • Machapisho
    • Katiba ya JMT
    • Sheria ndogo ndogo za Halmashauri
    • Hotuba Mbalimbali
    • Sera ya Elimu
    • Taarifa za Hesabu za Mwisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WANANCHI GAIRO WAJITOKEZA KUCHANJWA CHANJO YA UVIKO-19

Posted on: August 5th, 2021

Wilaya ya Gairo imezindua rasmi zoezi la chanjo ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya UVIKO-19 linalo endelea nchi nzima, ambapo wakazi wa maeneo mbalimbali ya Mji wa Gairo wamejitokeza kwa shauku kubwa kushiriki kuchanjwa.

Kwa mara ya kwanza nchini Tanzania, chanjo ya UVIKO-19 ilizinduliwa Ikulu Jijini Dar es Salaam Julai 28 2021 na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo katika hotuba yake Mhe. Rais aliwambia Watanzania kuwa swala la uchanjwaji ni la hiari hakuna mamlaka yoyote ya Serikali au binafsi itakayo mshurutisha mtu kuchanjwa.

Wakazi wa Mji wa Gairo wamepokea zoezi la chanjo ya UVIKO kwa ari ya kipekee kwa kuonyesha mwamko na hamasa kubwa ya kuhitaji huduma ya chanjo hali ambayo imeelezwa kuwa ufahamu kuhusu chanjo na kinga ya UVIKO imeongezeka kwa wananchi walio wengi.

Akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mheshimiwa Jabiri Omari Makeme, Katibu Tawala a Wilaya ya Gairo Bwana Augustino Chazua aliwataka wananchi kuendelea kupuuza taarifa za upotoshaji zinazo sambazwa na baadhi ya Wananchi kwamba kinga hiyo ya UVIKO-19 ina madhara makubwa kwa binadamu.

“Yapo maneno maneno ya upotoshaji yanasambaa mitaani na kwenye mitandao ya kijamii hukusu kuwepo na madhara kwenye chanjo hizi za JJ, wapuuzeni hao kwani hawaitakii mema nchi yetu wala hawapendi kuona tunavuka salama katika janga hil”. Alisisitiza Chazua.

Bwana Chazua alibainisha kuwa Viongozi wa Wakuu wa Nchi wakiongozwa na Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan wamekuwa mstari wa mbele kusisitiza usalama wa chanjo na wamekuwa mfano kwa kuwa wa kwanza kuchoma chanjo hivyo siyo jambo rahisi kukubali kupata chanjo ambazo zinahisiwa kuwa na madhara kwa binadamu.

“Tumeshuhudia wenyewe jinsi Mama yetu kipenzi akichoma chanjo kwa uwazi tena bila chembe ya shaka. Hivi ni kiongozi gani anayeweza kuweka rehani uhai wake kwa kukubali kuchomwa chanjo ambayo inamadhara”. Alihoji katibu Tawala huyo.

Hata hivyo aliwasisitiza Wananchi kuendelea kuchukua tahadhali na kuongeza juhudi ya udhibiti wa kuzuia maambukizi UVIKO, na kuwakumbusha kukaa mbalimbali, Uvaaji wa maski, unawaji wa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kutokusalimiana kwa kushikana mikono sambamba na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.

Serikali imetoa muongozo wa utoaji wa chanjo ya UVIKO ambapo itakuwa ni ya hiari na vipaumbele ni makundi ya watu watumishi wa sekta ya Afya, watu wazima umri wa miaka 50 na kuendelea na watu wenye magonjwa sugu ya muda mrefu.

 Kimkoa, Morogoro ilizindua chanjo ya UVIKO mnamo Agosti 3, 2021, huku Wilaya ya Gairo nayo ikitekeleza agizo hilo kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika chanjo dhidi ya virusi vinavyo sababisha korona Agosti 5.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWEYE USAILI WAOMBAJI NAFASI ZA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI III NA DEREVA II September 21, 2024
  • TANGAZO LA HALMASHAURI KUKUSANYA USHURU WA USAFI May 07, 2024
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA PROGRAM YA BBT May 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA MAAFISA WATENDAJI WA VIJIJI NA DEREVA July 12, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AFUNGUA TAWI LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR MKOA WA MOROGORO

    July 17, 2024
  • GAIRO SEKONDARI YATEKELEZA AGIZO LA KULIMA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA, MATUNDA

    July 15, 2024
  • MARUFUKU KUUZA, KUNUNUA MAZAO KWA KUPIMA KWENYE NDOO, MADEBE

    July 12, 2024
  • KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI

    July 11, 2024
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAASWA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni za Manunuzi
  • Zabuni za Ujenzi
  • Huduma

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Tanzania
  • GAIRO ONLINE TV
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Mawasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Gairo-Mtaa wa Malimbika, Kata ya Gairo.

    Sanduku la Posta: 40, GAIRO

    Simu ya Mezani: +255 787730665

    Simu ya Kiganjani: +255 717222572

    Barua pepe: ded@gairodc.go.tz, info@gairodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo. Haki Zote Zimehifadhiwa